![]() |
Wachezaji wa Zanzibar Heroes |
TIMU ya soka ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes imerejea
nchini jana ikitokea Uzbekistan ilikokuwa ikishiriki michuano ya Kombe la Dunia
ya VIVA, inayohusisha nchi ambazo si wanachama wa Shirikisho la Soka la
Kimataifa (FIFA) na kuambulia Medali ya Shaba.
Zanzibar ilishinda Medali hiyo, baada ya Jumapili kuifunga
Province ya Ufaransa mabao 7-2 katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu.
Awali, katika mchezo wa Nusu Fainali, Zanzibar ilifungwa
mabao 2-0 na Cyprus na Kaskazini, hivyo kukosa tiketi ya kucheza Fainali.
Katika mechi za Kundi lake A, Zanzibar ilifanikiwa kutinga
Nusu Fainali baada ya kuzifunga Ratia 6-0 na Elaam 3-0.
Wachezaji wa Zanzibar sasa watarejea kwenye klabu zao, kabla
ya kuitwa tena baadaye kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
Mashariki na Kati, Challenge, ambayo hufanyika kila mwishoni mwa mwaka.
0 comments:
Post a Comment