• HABARI MPYA

    Monday, October 15, 2012

    CAMEROON NJE TENA MATAIFA YA AFRIKA, YATOLEWA NA CAPE VERDE

    Cameroon

    CAMEROON imekosa tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani kwa mara ya pili mfululizo, baada ya visiwa vya Cape Verde kwa jumla ya mabao 3-2. Jana Camroon imeshinda mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano dhidi ya Cape Verde mjini Yaunde.
    Ikumbukwe Cape Verde iliilaza Cameroon 2-0 katika mechi yao kwanza, hivyo wenyeji jana walitakiwa washinde si chini ya 3-0 ili kusonga mbele.
    Cape Verde sasa imeweka historia kwa kufuzu mara ya kwanza kwenye fainali hizo za kuwania kombe la Mataifa Afrika, zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
    Katika mechi nyingine ya kufuzu, Ethiopia ilivaana na Sudan ambapo Ethiopia imeibuka na ushini wa mabao 2-0. Katika mechi ya kwanza Sudan ilishinda 5-3. Ethiopia sasa imufuzu kupitia kwa sheria ya bao la ugenini baada ya timu hizo kufungana jumla ya mabao 5-5.
    Mechi kati ya Senegal na Ivory Coast ilivunjika juzi baada ya mashabiki wa soka kuzua ghasia wakati wa mechi hiyo mjini Dakar.
    Mashabiki hao wa Senegal, waliwasha moto na kuanza kurusha mawe uwanjani wakati Ivory Coast, ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-0, matokeo ambayo yangeiondoa timu yao. Mashabiki wa Ivory Coast, walilazimika kuingia uwanjani ili kukwepa ghasia hizo.
    Wachezaji na mashabiki hao wa Ivory Coast walisindikizwa na Polisi wa kupambana na ghasia ambao walirusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya mashabiki wa Senegal.
    Ripoti zinasema watu 10 akiwemo Waziri wa Michezo wa Senegal, Hadhi Malick Gakou, walijeruhiwa kwenye vurugu hizo zilizotokea katika Uwanja wa Leopold Sedar Senghor.
    Ghasia hizo zilianza wakati mshambuliaji nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba, alipofunga bao lake la pili kwa mkwaju wa penalti, huku zikiwa zimesalia dakika 15 mechi hiyo kumalizika.
    Kama mechi hiyo ingelimalizika matokeo yakiwa hivyo, Ivory Coast ingeliibuka na ushindi wa jumla wa mabao 6-2 na kusonga mbele.
    Shirikisho la Soka Afrika (CAF) halijatoa taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo, lakini maafisa wa Shirikisho la Soka Senegal, wamesema, timu hiyo ya Senegal huenda ikaadhibiwa vikali na CAF.

    MATOKEO KAMILI NA TIMU ZILIZOFUZU:
    Ethiopia 2-0 Sudan - Addis Ababa
    Matokeo ya Jumla: Sudan 5-5 Ethiopia
    Ethiopia wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini

    Cameroon 2-1 Cape Verde  -Yaounde-
    Matokeo ya Jumla: Cape Verde 3-2 Cameroon
    Cape Verde wamefuzu kwa mara ya kwanza fainali zijazo za Afcon 2013 kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2.

    Angola 2-0 Zimbabwe – Luanda
    Matokeo ya Jumla: Angola 3-3 Zimbabwe
    Angola wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini.

    MECHI ZA JUMAMOSI (Oktoba 13, 2014)
    Malawi 0-1 Ghana - Lilongwe
    Matokeo ya Jumla: Ghana 3-0 Malawi
    Ghana imefuzu kwa mara nyingine

    Botswana 1-4 Mali - Gaborone
    Matokeo ya Jumla: Mali 7-1 Botswana
    Mali imefuzu

    Uganda 1-0 Zambia - Kampala
    Matokeo ya Jumla: Uganda 1-1 Zambia
    Zambia wameshinda kwa penalti 9-8 na kufuzu

    Nigeria 6-1 Liberia - Calabar
    Matokeo ya Jumla: Nigeria 8-3 Liberia
    Nigeria imefuzu

    Tunisia 0-0 Sierra Leone - Monastir
    Matokeo ya Jumla: Sierra Leone 2-2 Tunisia
    Tunisia wamefuzu kwa faida ya mabao ya ugenini

    Senegal 0-2 Ivory Coast - Dakar
    Mechi imevunjwa kwa sababu ya vurugu za mashabiki

    Matokeo: Morocco 4-0 Msumbiji - Marrakech
    Matokeo ya Jumla: Msumbiji 2-4 Morocco
    Morocco imefuzu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CAMEROON NJE TENA MATAIFA YA AFRIKA, YATOLEWA NA CAPE VERDE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top