• HABARI MPYA

    Friday, March 02, 2012

    LILLIAN INTERNET ACHOKA KUTWANGA NA KUPEPETA, AAMUA KUWA SHUJAA


    BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa Musica, imezidi kuibomoa bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ baada ya kumnyakua  mnenguaji wake mahiri, Lillian Tungaraza maarufu kama ‘Lilli Internet’.
    Aidha, Mashujaa pia imemuongeza katika safu yake mpapasa gitaa la solo ambaye alipata kuzitumikia bendi kadhaa ikiwemo Twanga, Pepeta, Ally Akida
    Akizungumza mjini Dar es Salaam jana, Meneja wa Mashujaa Band Maximilian Luhanga alisema kwamba wameamua kuwachukua wanamuziki hao ili kuimarisha bendi yao katika idara hizo.
    Alisema pamoja na kuimarisha idara hizo pia, wanaamini uzoefu na umahiri walionao wasanii hao utasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza kiwango cha bendi yao ambayo kwa sasa imeingia rasmi katika ushindanmi wa kimuziki.
    Aliongeza kuwa tayari wasanii hao wameshasaini mikataba ya kuitumikia bendi hiyo kwa miaka miwili na Jumatano watapanda kwenye jukwaa la bendi hiyo kwa mara ya kwanza katika ukumbi wa Nyumbani Lounge.
    Hii ni mara ya pili kwa Mashujaa kuibomoa Twanga Pepeta, kwani mapema mwaka huu ilimnyakua Charles Gabriel ‘Chaz Baba’.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LILLIAN INTERNET ACHOKA KUTWANGA NA KUPEPETA, AAMUA KUWA SHUJAA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top