• HABARI MPYA

    Tuesday, May 08, 2012

    GWIJI MWINGINE WA SOKA AFRIKA AFARIKI DUNIA


              
       
    CAF President mourns the death of Senegal legend Bocande

    RAiS wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Issa Hayatou ameelezea mshituko wake kufuatia kifo cha gwiji wa soka Senegal, Jules Francois Bocande (pichani kushoto).
    Mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba wa Teranga, amefariki dunia jana (Mei 7) mjini Metz, Ufaransa akiwa na umri wa miaka 53, baada ya kufanyiwa upasuaji.
    Hayatou amekizungumzia kifo hicho kama pigo linguine kwa soka ya Afrika, kufuatia kifo cha mshambuliaji wa zamani wa Nigeria, Rashidi Yekini mwishoni mwa wiki.
    Hakuna shaka Bocande, alikuwa miongoni mwa vipaji vya hali ya soka vilivyowahi kutokea Magharibi mwa Afrika na kifo chake kimekuja saa 72  baada ya kufariki kwa Rashidi Yekini.
    Mshambujliaji huyo alijitengenezea jina nchini Ufaransa ambako alicheza soka kati ya mwaka 1985 hadi 1986 akifunga mabao 23 katika klabu ya Metz. Pia alichezea Paris Saint-Germain, OGC Nice na RC Lens.
    Baada ya kustaafu soka, alikuwa kocha wa muda wa Simba wa Teranga kati ya mwaka 1994 na 195, sambamba na kuwa Mswaidizi wa Mfaransa, Bruno Metsu katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2002 ambako Senegal ilitinga Robo Fainali.
    Mwaka 2009, alitajwa kwenye orodha ya CAF ya magwiji wa soka Afrika, sambamba na Stephen Keshin wa Nigeria na Osvaldo Saturnino de Oliviera “Jesus” wa Angola katilka tuzo za Gala zilizofanyika Accra, Ghana 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GWIJI MWINGINE WA SOKA AFRIKA AFARIKI DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top