• HABARI MPYA

    Tuesday, May 08, 2012

    MWAMBA AISINDIKIZA SIMBA SUDAN


    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linaitakia kila la kheri timu ya Simba kwenye mechi yake ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika, dhidi ya Al Ahly Shandy ya Sudan itakayochezwa Jumapili (Mei 13 mwaka huu).
    Mechi hiyo itachezwa katika mji wa Shandy kuanzia saa 2 kamili usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Simba inaondoka kesho kwenda huko kwa ndege ya Kenya Airways.
    Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY leo mchana kwamba  msafara wa timu hiyo utaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Hussein Mwamba, na unatarajia kurejea nyumbani Mei 15 mwaka huu.
    Pia TFF inaipongeza Simba kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ambayo Mei 6 mwaka huu ilifunga msimu wa 2011/2012.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MWAMBA AISINDIKIZA SIMBA SUDAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top