![]() |
| Tevez na Silba kushoto |
SAWA soka inaundwa na maajabu, lakini sijui
kama hilo
linaweza kutokea hapa. Ni katika vita ya ubingwa wa Ligi Kuu England kwa
msimu huu.
Haitashangaza kama Ligi Kuu itaanza
kulipamba kwa vitambaa vya rangi ya bluu taji hilo , wakisubiri kufikisha Etihad Stadium
Jumapili hii ili kukabidhiwa wenyewe ‘mwali’ wao.
Labda tetemeko la ardhi au masahibu mengine
ya mwenyezi Mungu ndiyo yatakayoizuia Manchester City
kutawazwa mabingwa kwa mara ya kwanza baada ya kusubiri kwa miaka 44.
Wapinzani wao? Kikosi cha QPR – ambacho
kitaamua hilo inanolewa na Mark Hughes, kocha
aliyetimuliwa kiutata na Man
City kumpisha Roberto
Mancini.
Na rekodi yao
ya ugenini kwa msimu huu kwa kikosi hicho cha QPR, hakuna atakayetoa sarafu
yake kwa upande wa Man
City kunyakua ubingwa huo.
Baada ya mabao maridadi kabisa katika
kipindi cha pili yaliyofungwa na Yaya Toure dhidi ya Newcastle
juzi, kwa sasa njia safi
kabisa Etihad kumpokea ‘mwali’ huyo.
Hakika, ilikuwa ni siku njema kabisa kwa
nyota huyo wa Ivory Coast
– aliyesherehekea ‘birthday’ yake kwa kutimiza miaka 29.
Ilikuwa ni siku ya kukumbukwa kwa mchezaji
huyo ambaye aliwapa shangwe mashabiki wa klabu hiyo kwa mara ya kwanza tangu 1968.
![]() |
| Mancini nyuma ya Balotelli |
Usiku wa juzi, bado Mancini aliendelea
kupuuza kwamba ubingwa ni wao msimu huu, licha ya mpinzani wake kocha wa
Manchester United, Alex Ferguson kudai kwamba Man
City imeweka “mikono miwili” kwenye
taji hilo .
“Hakuna kilichoamriwa hadi sasa,” alisema
Muitaliano huyo. “Tuna mechi nyingine ngumu Jumapili ijayo — kama
ilivyokuwa leo (juzi).”
QPR wagumu? Si timu ya kubeza, Roberto Mancini
— napaswa kulitambua hilo
na kufahamu kwamba heshima ya mashabiki wa City isije ikachafuka mwisho wa
mchezo wa Jumapili hii.
Kama kuna timu ambayo unaweza kucheza dhidi
yao na kuwa na
uhakika wa kunyakua taji ni QPR — licha ya kwamba kikosi hicho kinahitaji
pointi moja kujinusuru kutoka kwenye hatari ya kushuka daraja.
Klabu hiyo ya London Magharibi imekuwa na
rekodi ya kupoteza mechi nyingi za ugenini — mechi 13 — ikiwa ni zaidi ya timu
yoyoye kwenye ligi hiyo.
Tangu walipopata ushindi wao wa mwisho
dhidi ya Stoke, Novemba 19, wamepoteza mechi 10 na kutoka sare mbili katika
mechi zao za 12 za hivi karibuni walizocheza nje ya Loftus Road.
Kwa mtazamo huo na Man
City ikiwa ilipata sare kwenye mchezo
wao wa pili wa ligi msimu na kushinda zote walizocheza nyumbani — kwa hilo ile subira ya muda
mrefu imefika ukingoni.
![]() |
| Tevez na Balotelli |
Baada ya kufunga bao la pili, Yaya Toure
alikuwa na uhakika mkubwa kwamba kikosi hicho kimeonyesha bayana kuhusu uwezo
wao wa kunyakua ubingwa kwa msimu huu.
Mashabiki wa Man City
wakawa na uhakika na kuimba: “Na sasa mmetuamini....tunakwenda kunyakua ubingwa
wa ligi.”
Bao hilo la
pili lilibainisha kila kitu kwamba huu ni msimu mzuri kabisa kwa Man City na
hakuna kitachoweza kuwazuia katika kutimiza ndoto yao ya kunyakua ubingwa.
Wakati walipoweza kuifunga Newcastle
kwa ‘counter-attack’, City ilionyesha kuwa na uchu wa kufunga baada ya kwenda
mbele wachezaji wanne dhidi ya wawili wa Newcastle .
Sergio Aguero, alikimbia na mpira upande wa
kushoto, akamtafuta Nigel de Jong, aliyepiga ndefu kwa Gael Clichy – beki huyo
wa pembeni alimpenyezea Yaya Toure, ambaye alitulia na kumchambua kipa Mdachi Tim
Krul.
Kwenye benchi lao, David Platt alionekana
kuchanganyikiwa, Mancini alipiga ngumi upepo na Brian Kidd alichofanya ni
kuangusha tabasamu tu.
Kilikuwa kipindi chao cha kufurahi na
kusahau kilio cha 1993 – wakati walipobanwa Old Trafford na kikosi cha Alex
Ferguson kikifanikiwa kunyakua ubingwa kwa mara ya kwanza baada ya miaka 26.
Baada ya kuona timu yao
inapata ushindi safi
katika mechi hiyo ngumu kabisa, waliamini hakuna kitachoweza kuwazuia katika
kunyakua ubingwa huo msimu huu.
Ilikuwa siku mbaya kwa Newcastle – kwasababu walitambulisha sanamu
ya gwiji wao, Bobby Robson na kisha wanakumbana na kichapo.
Baada ya kichapo kutoka kwa Arsenal –
ilikuwa ni siku ambayo Mancini aliamini kwamba ubingwa tena kwao basi, lakini
baada ya United kuteleza na kisha kufanikiwa kuwafunga kwa sasa kila kitu kipo
mikononi mwao.
![]() |
| Kun Aguero |
City kwa sasa itaamua yenyewe, kunyakua
taji au kulitoa sadaka kwa mahasimu wao United kwa maana ya kushindwa kupata
ushindi katika mchezo wao wa mwisho dhidi ya QPR.






.png)
0 comments:
Post a Comment