• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    MARK HUGHES ASEMA HAENDI KULIPA KISASI CHA KUFUKUZWA ETIHAD,


    Mark Hughes
     Mark Hughes 
    Published: Today at 15:43

    MARK HUGHES amesema kwamba hataitumia mechi kati ya timu yake, QPR dhidi ya Manchester City kwa vita zake binafsi.

    Rangers wanahitaji pointi moja tu, kuzima ndoto za Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Jumapili, iwapo Manchester United wataifunga Sunderland- nao kujihakikishia kubaki Ligi Kuu.
    Lakini mechi hiyo itakayopigwa Etihad imekuwa gumzo kubwa, baada ya Hughes kufukuzwa ‘kinyama’ na City mwaka 2009 na nafasi yake kuchukuliwa na Roberto Mancini.
    Hughes, pamoja na hayo amekataa kuitumia mechi hiyo kama sehemu ya kulipa kisasi.
    Alisema: “Watu wamekuwa wakisema maneno hayo, lakini siyo mawazo yangu kabisa.
    “Pointi yangu ni kuangalia kikamilifu juu ya kipi tunatakiwa kufanya, kama ambavyo ungetarajia.
    “Tunakabiliwa na mchezo mkubwa na mgumu. Haitakuwa rahisi kwa Manchester City kama timu imara.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MARK HUGHES ASEMA HAENDI KULIPA KISASI CHA KUFUKUZWA ETIHAD, Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top