• HABARI MPYA

    Thursday, July 12, 2012

    AZAM ACADEMY NAYO YAFUNGWA BURUNDI


    LEO haikuwa siku nzuri kwa Azam kwa ujumla. Wakati Azam A ikiukosakosa ubingwa wa Kombe la Urafiki, kwa kufungwa na Simba SC, Dar es Salam, timu ya soka ya vijana ya Azam FC, Azam Academy leo imefungwa 1-0 kwenye michuano ya Rollingston inayoendelea nchini Burundi, katika mechi ambayo mgeni rasmi alikuwa rais wa Burundi, Perre Nkurunziza.
    Hata hivyo, kipigo hicho hakiiathiri Azam, kwani tayari imekwishafuzu Robo Fainali, baada ya kushinda mechi zake mbili za awali 1-0 dhidi ya Kyazanga FC ya Uganda na 3-0 dhidi ya Nyirakongo Academy ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    Azam sasa itamenyana na Mjini Magharibi katika Robo Fainali ya michuano hiyo, Jumanne.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM ACADEMY NAYO YAFUNGWA BURUNDI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top