• HABARI MPYA

    Saturday, July 14, 2012

    NGORONGORO NA NYIGU WADOGO CHAMAZI LEO


    Thomas Ulimwengu wa Ngorongoro

    Na Princess Asia
    TIMU ya taifa ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes, leo inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Chamazi, kumenyana na vijana wenzao wa Rwanda katika mchezo wa kirafiki, kujiandaa na mechi dhidi ya Nigeria Julai 29, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika.
    Rwanda ‘Nyigu Wadogo’, waliwawasili Dar es Salaam jana mchana Dar es Salaam kwa ndege ya shirika la ndege la Rwanda kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki dhidi ya Ngorongoro Heroes.
    Rwanda yenye msafara wa watu 27 wakiwemo wachezaji 20, imefikia katika hoteli ya Sapphire na baada ya mechi ya leo, timu hizo zitacheza tena keshokutwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Ngorongoro Heroes iko kambini chini ya Kocha wake, Mdenmark Jakob Michelsen na msaidizi wake Mohamed Adolf Rishard.
    Mechi dhidi ya Nigeria ambayo ni ya kwanza ya raundi ya pili kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Algeria itachezwa Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NGORONGORO NA NYIGU WADOGO CHAMAZI LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top