 |
Kikosi cha Yanga |
Na
Mahmoud Zubeiry
MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la
Kagame, Yanga SC ya Dar es Salaam, watacheza mechi ya kwanza katika ziara yao
nchini Rwanda kesho Uwanja wa Amahoro mjini Kigali, dhidi ya mabingwa wa zamani
wa Afrika Mashariki na Kati pia, Rayon Sport.
Leo Yanga watatembelea Ikulu ya Rwanda, walipoalikwa
na rais Paul Kagame kupeleka Kombe la Afrika Mashariki na Kati, ambalo tangu
mwaka 2002 mfadhili wake mkuu na mlezi wake ni Rais Kagame.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah
Ahmad Bin Kleb ameiambia BIN ZUBEIRY kwa simu kutoka Kigali
kwamba, timu hiyo baada ya kufika nchini humo jana, ilifanya mazoezi kwenye
Uwanja wa Nyamirambo na leo asubuhi itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Amahoro.
Bin Kleb alisema kwamba Yanga itashuka dimbani
kumenyana na Polisi Jumapili na kwa mujibu wa ratiba ya awali, wanatakiwa
kurejea Dar es Salaam Jumatatu.
Hata hivyo, Bin Kleb alisema wanafanya mipango ya
kurefusha ziara yao nchini humo na kama watafanikiwa watacheza mechi
zaidi.
Awali, Yanga ilikuwa icheze pia na mabingwa wengine
wa zamani wa Kombe la Kagame, APR, lakini kutokana na timu hiyo kukabiliwa na
mgogoro hivi sasa uliosababisha kufukuzwa kwa kocha Mholanzi, Ernest Brandy na
nafasi yake kupewa kocha mzalendo kwa muda, imeshindwa kucheza.
Katika ziara hiyo, Yanga haijaambatana na mfungaji
bora wa Kombe la Kagame, Said Bahanuzi ambaye amebaki Dar es Salaam kwa
matatizo ya kifamilia. Yanga imekwenda Rwanda na msafara wa watu 42, wakiwemo
wachezaji 28, Maofisa watano wa benchi la Ufundi na viongozi wanane.
Viongozi walio na timu Kigali ni Mwenyekiti, Yussuf
Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini Mama
Fatma Karume, Francis Kifukwe na Seif Ahmed ‘Magari’ sambamba na Wajumbe wa
Kamati ya Utendaji, Abdallah Bin-Kleb na Salum Rupia.
Benchi la ufundi ni kocha mkuu; Tom Saintfiet, Kocha
Msaidizi Fred Felix Minziro, Meneja Hafidh Saleh, Daktari, Sufiani Juma na
Mtunza vifaa Mahmoud Omary ‘Mpogolo’, wakati wachezaji ni makipa: Yaw Berko,
Ally Mustafa ‘Barthez’ na Said Mohamed. Mabeki Shadrack Nsajigwa, Godfrey
Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, Stefano Mwasyika, David Luhende, Nadir Haroub
‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Ibrahim Job, Ladisalus Mbogo; viungo Athumani Iddi
‘Chuji’, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Simon Msuva, Shamte Ally, Omega
Seme, Idrisa Rashid, Nizar Khalfan, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Rashid
Gumbo, Nurdin Bakari na washambuliaji; Hamis Kiiza ‘Diego’, Jerry Tegete na
Didier Kavumbangu.
Yanga ilitwaa Kombe la Kagame kwa mara ya pili
mfululizo wiki mbili zilizopita, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa kuifunga
Azam FC mabao 2-0, ambayo yalitiwa kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego Milito’ na
Said Bahanuzi ‘Spider Man’.
Hiyo kwa ujumla ilikuwa mara ya tano mfululizo,
Yanga inatwaa Kombe hilo, baada ya awali kuchukua mwaka jana, wakiifunga Simba
katika fainali bao 1-0, Uwanja wa Taifa mfungaji Kenneth Asamoah ambaye
ametemwa, ingawa siku hiyo Kiiza pia alifunga bao safi, ambalo refa alilikataa.
Yanga ilichukua kwa mara ya kwanza Kombe hilo, mwaka
1975 ikiifunga tena Simba katika fainali, mabao 2-0 wafungaji Sunday Manara
‘Computer’ na Gibson Sembuli (sasa marehemu) Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Ikachukua tena mwaka 1993, Uwanja wa Nakivubo,
Kampala, Uganda kwa kuifunga SC Villa mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Said Nassor
Mwamba ‘Kizota’ (sasa marehemu) na Edibily Jonas Lunyamila.
Ilichukua tena mwaka 1999, ikiifunga tena SC Villa,
Uwanja wa Nakivubo, kwa penalti 5-3, kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120,
Yanga ikisawazisha bao kupitia kwa Lunyamila, baada ya Hassan Mubiru kutangulia
kuifungia Villa, siku hiyo Manyika Peter akicheza penalti mbili za
Waganda.
Aidha, kwa kutwaa Kombe hilo chini ya Mbelgiji huyo,
Yanga imeendeleza rekodi yake ya kutwaa mataji ya michuano hiyo, chini ya
makocha wa kigeni baada ya mwaka 1975 kuchukua chini ya Tambwe Leya aliyekuwa
raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kabla ya kuchukua uraia wa
Tanzania, (sasa marehemu), 1993 chini ya Nzoyisaba Tauzany aliyekuwa raia wa
Burundi kabla ya kuchukua uraia wa Tanzania, mwaka 1999 chini ya Raoul Shungu
wa DRC na mwaka jana chini ya Mganda, Sam Timbe.
 |
Rais Kagame akisalimiana na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Yanga, Mama Fatma Karume |
 |
MEZA YA MAPROO; Hapa kuna Mbuyu Twite, Hamisi Kiiza aliyeipa mgongo kamera, Didier Kavumbangu kushoto na Yaw Berko anayetazajma kamera |
 |
Wachezaji |
 |
Rais Kagame akisalimiana na kocha wa Yanga, Tom Saintfiet |
 |
Wachezaji wa Yanga wakims |
 |
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' akiwa na kocha Saintfiet, wakimkabidhi Kombe Rais Kagame |
 |
Mwenyekiti wa Yanga, Yussufr Manji akizungumza kitu mbele ya rais Kagame |
 |
Sief Ahmad Magari akimkabidhi jezi ya Yanga Rais Kagame mbele ya Mama Fatma Karume |
 |
Rais Kagame akizungumza na Yanga |
 |
Rais Kagame akizungumza na Mwenyekiti wa Yanga, Manji |
 |
Rais Kagame katika picha ya pamoja na Yanga. PICHA ZOTE NA SALEH ALLY, MHARIRI KIONGOZI GAZETI LA CHAMPIONI |
0 comments:
Post a Comment