• HABARI MPYA

    Sunday, September 09, 2012

    SIMBA WAMTEKA YONDAN KIMAFIA, YANGA WAMKOMBOA KIKOMANDOO


    Yondan akisaini Yanga.
    INADAIWA beki wa Yanga, Kevin Yondan ametekwa na klabu yake ya zamani, Simba SC leo katika kile kinachoelezwa jitihada za kumrudisha nyumbani.
    Inadaiwa mchezaji wa zamani wa Simba SC, ameongoza zoezi hilo la kumnasa Yondan na kumkutanisha na viongozi wa Simba.
    Yondan hakupatikana kwenye simu yake alipotafutwa na BIN ZUBEIRY usiku huu, lakini Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb alipatikana na akasema; “Nipo nje ya nchi, ila taarifa hizo ni kweli, lakini na sisi kwa ushirikiano wa mchezaji mwenyewe, tulifanikiwa kumkomboa mchezaji huyo na tumefungua kesi dhidi ya wahusika," alisema Bin Kleb.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WAMTEKA YONDAN KIMAFIA, YANGA WAMKOMBOA KIKOMANDOO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top