• HABARI MPYA

    Thursday, January 10, 2013

    YANGA WACHEZA NA WAHOLANZI KESHO

    Brandts akiwanoa wachezaji wake Uturuki

    Na Baraka Kizuguto, Antalya
    Timu ya Young Africans Sports  Club kesho itashuka dimbani kucheza mchezo wake wa mwisho na wa tatu (3) dhidi ya  timu ya Emmen FC ya ligi daraja la kwanza nchini Uholanzi  katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika katika viwanja vya Adora football - Berek pembeni kidogo ya mji wa Antlaya.
    Young Africans ambayo imeshakaa takribani siku 12 katika mji wa Antalya na kucheza michezo miwili ya kirafiki dhidi ya timu za Armini Bielefeld ya Ujerumani na Denizlispor ya Uturuki leo asubuhi imeendelea na mazoezi katika viwanja vya Fame Residence football mjini Antalya.
    Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema atatumia mchezo huo wa mwisho kama fursa pekee kwao kwani mchezo huo utakuwa kipimo kizuri kwao kwani timu ya Emmen FC ni timu nzuri na ndio maana ipo katika ligi daraja la kwanza nchini Uholanzi.
    Akiongelea mchezo huo wa kesho  Brandts amesema timu ya Emmen FC ni timu nzuri, imekuja Antalya kuweka kambi ya mafunzo kujiandaa na mzunguko wa ligi daraja la kwanza nchini Uholanzi, hivyo ni nafasi nzuri ya kujipima uwezo na timu hiyo ya Uholanzi.
    Young Africans inatarajia kuondoka mjini Antalya siku ya jumapili mchana kupitia Istambul ambapo itaondoka majira ya saa 1 usiku, saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki na inatarajiwa kufika Dar es salaam Tanzania majira ya saa 10 usiku kasoro.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA WACHEZA NA WAHOLANZI KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top