IMEWEKWA AGOSTI 16, 2013 SAA 7:43 MCHANA
KLABU ya Chelsea bado ina dhamira ya kumsajili mshambuliaji wa Anzhi Makhachkala, Samuel Eto'o.
The Blues kwa sasa wanataka straika, staa wa Manchester United, Wayne Rooney ndiyo chaguo la kwanza la kocha Jose Mourinho.
Eto'o alishinda ligi ya mabingwa akiwa na Inter Milan mwaka 2010 akicheza chini ya Mourinho.

Anataka kuondoka: Samuel Eto'o amepania kuondoka Anzhi Mackhachkala na Chelsea ikipewa nafasi ya kumnasa.
Mapema wiki hii gwiji huyo wa Cameroon alikiri kwamba anataka kucheza chini ya kocha wa Chelsea.
Alisema: “Kuna Jose Mourinho mmoja tu. Nimecheza chini ya makocha wengi wazuri – lakini hakuna mwenye tabia kama za Jose.
“Ni mmoja kati ya makocha bora duniani – na tulifanikiwa sana tulipokuwa pamoja Inter Milan. Ningependa kucheza chini yake tena – kwa sababu huchoki kuwa pembeni ya Jose.
“Ndio Chelsea ni timu bora – na tutakapopata ofa zote mezani, hapo nitazungumza na wakala wangu na kujua hatua yangu nyingine.”
Hatahivyo, Dynamo Moscow wamewasajili wachezaji wenzake Igor Denisov, Yuri Zhirkov na Aleksandr Kokorin.

Anasepa: Staa wa zamani wa Chelsea, Yuri Zhirkov (kushoto) ameondoka Anzhi na kutua Dynamo Moscow.

Mzigo wa Italia: Jose Mourinho aliiongoza Inter Milan kuchukua taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2010 kwa msaada wa Eto'o