• HABARI MPYA

    Saturday, July 19, 2014

    JOHN TERRY ATOKEA BENCHI NA KUINUSURU CHELSEA KULALA KWA TIMU YA 'MCHANGANI'

    NAHODHA John Terry amempa raha kocha Jose Mourinho, kwa kuipa Chelsea ushindi wa 3-2- akifunga mabao mawili dhidi ya timu ya Daraja la pili, AFC Wimbledon.
    Timu hiyo ya Ligi Kuu ilikuwa nyuma zikiwa zimesalia dakika 16 kutokana na kazi nzuri ya Ade 'The Beast' Akinfenwa, lakini kuingia kwaTerry na Branislav Invanovic kulibadilisha matokeo.
    The Blues ilidondoshwa na mabao ya Alan Bennett kwa kichwa dakika ya 40 kabla ya Matt Tubbs kumtungua kwa penalti, Mark Schwarzer.
    Terry alipunguza bao la kwanza na Mohamed Salah akasawazisha zikiwa zimesalia dakika saba kabla ya Nahodha JT kufunga la ushindi.
    Super sub: John Terry akienda hewani kuifungia Chelsea bao la ushindi dhidi ya AFC Wimbledon Uwanja wa Kingsmeadow
    Mobbed: Terry is congratulated by his team-mates after finding the back of the net for a second time
    Terry akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la ushindi

    Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Schwarzer/Beeney, Zouma/Terry, Ake/Ivanovic, Christiansen/Chalobah, Bamford/Da Silva, Baker, Aina/Brown, Salah, Van Ginkel/Houghton, Swift/Romeu na Matic/Solanke.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JOHN TERRY ATOKEA BENCHI NA KUINUSURU CHELSEA KULALA KWA TIMU YA 'MCHANGANI' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top