MSHAMBULIAJI wa kimataifa nwa Ufaransa, Karim Benzema ameongeza mkataba wa kuendelea kuichezea Real Madrid hadi mwaka 2019 baada ya kukataa kuhamia timu za Ligi Kuu ya England.
Kulikuwa kuna tetesi kwamba mpachika mabao huyo wa Ufaransa anaweza kuondoka klabu hiyo ya Hispania, lakini sasa wazi ataishi Bernabeu hadim mwaka 2019.
Arsenal, Liverpool na Tottenham Hotspur ni miongoni mwa timu za Ligi Kuu England zilizokuwa zinamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26.
0 comments:
Post a Comment