• HABARI MPYA

    Wednesday, November 12, 2014

    VAN PERSIE KUIKOSA MECHI YA UHOLANZI NA MEXICO LEO

    MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Robin van Persie ataikosa mechi ya kirafiki ya kimataifa baina ya nchi yake, Uholanzi dhidi ya Mexico Jumatano ya leo baada ya kocha Guus Hiddink kuthibitisha hayuko fiti kiasi cha kutosha.
    Van Persie akiwa Nahodha wa Uholanzi, aliiongoza hadi nafasi ya tatu katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Brazil, lakini kikosi cha Hiddink kimekuwa na wakati mgumu tangu baada ya michuano hiyo, kikishinda mchezo mmoja tu katika mechi zao tatu za awali za kufuzu kwa Euro.
    Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye alicheza dakika zote 90 klabu yake Man United ikimenyana na Crystal Palace mwishoni mwa wiki iliyopita, anaweza akarejea kwa wakati kuivaa Latvia Jumapili.
    Robin van Persie leaves the Dutch training session with fitness coach Rene Wormhoudt on Tuesday
    Robin van Persie akiondoka kwenye mazoezi ya Uholanzi na kocha wa mazoezi ya viungo, Rene Wormhoudt jana
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN PERSIE KUIKOSA MECHI YA UHOLANZI NA MEXICO LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top