Na Alex Sanga, DAR ES SALAAM
KIPA namba moja na Nahodha wa Toto African ya Mwanza, Erick Ngwengwe (pichani kulia) ametangaza kuachana na timu hiyo iliyopanda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao.
Kipa huyo anayechukua Shahada ya pili ya elimu kwenye chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza, amesema ameamua kuachana na timu hiyo kutokana na mkataba wake uliokuwa ni kuipandisha daraja timu hiyo na baada ya
kufanya hivyo sasa rasmi ameachana na timu hiyo.
Ngwengwe amesema kwa sasa amerejea kwenye timu yake ya mtaani, Black Star inayoshiriki Ligi Daraja la Nne na pia amesema kama viongozi wa timu ya Toto watakubali
matakwa yake, atasaini tena kwenye timu hiyo ya Mtaa wa Kishamapanda katikati ya jiji la Mwanza.
Lakini kuna tetesi zinasema kipa huyo anaelekea Mwadui FC ya Shinyanga.
KIPA namba moja na Nahodha wa Toto African ya Mwanza, Erick Ngwengwe (pichani kulia) ametangaza kuachana na timu hiyo iliyopanda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao.
Kipa huyo anayechukua Shahada ya pili ya elimu kwenye chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza, amesema ameamua kuachana na timu hiyo kutokana na mkataba wake uliokuwa ni kuipandisha daraja timu hiyo na baada ya
kufanya hivyo sasa rasmi ameachana na timu hiyo.
Ngwengwe amesema kwa sasa amerejea kwenye timu yake ya mtaani, Black Star inayoshiriki Ligi Daraja la Nne na pia amesema kama viongozi wa timu ya Toto watakubali
matakwa yake, atasaini tena kwenye timu hiyo ya Mtaa wa Kishamapanda katikati ya jiji la Mwanza.
Lakini kuna tetesi zinasema kipa huyo anaelekea Mwadui FC ya Shinyanga.



.png)
0 comments:
Post a Comment