• HABARI MPYA

    Sunday, November 30, 2025

    SINGIDA BLACK STARS YAOKOTA POINTI YA KWANZA KOMBE LA SHIRIKISHO


    TIMU ya Singida Black Stars imetoa sara ya kufungana bao 1-1 na Stellenbosch ya Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi C Kombe la Shirikisho Afrika usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
    Stellenbosch ilikuwa ya kupata bao lililofungwa na mshambuliaji mzawa, Langelihle Phili dakika ya 52, kabla ya kiungo wa Kimataifa wa Togo, Marouf Tchakei kuisawazishia Singida Black Stars dakika ya 90’+1.
    Kwa matokeo hayo, Stellenbosch wanafikisha pointi nne na kurejea kileleni mwa Kundi C, mbele ya AS Otohô ya Kongo-Brazzaville yenye pointi tatu sawa na CR Belouizdad ya Algeria, wakati Singida Black Stars yenye pointi moja inashika mkia.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SINGIDA BLACK STARS YAOKOTA POINTI YA KWANZA KOMBE LA SHIRIKISHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top