• HABARI MPYA

    Wednesday, June 20, 2012

    BARTHEZ AANZA MAZOEZI RASMI YANGA JIONI HII


    Barthez

    Na Prince Akbar
    KIPA wa Simba, Ally Mustafa ‘Barthez’ ameanza mazaoezi jioni hii katika klabu yake mpya, Yanga SC kwenye Uwanja wa Kaunda, Dar es Salaam.
    Barthez ni miongoni mwa wachezaji 17 ambao hadi sasa tayari wapo Uwanja Kaunda wakijifua chini ya kocha Freddy Felix Minziro.
    Wengine ni Said Bahanuzi na Juma Abdul, wote kutoka Mtibwa Sugar ya Morogoro na Nizar Khalfan aliyekuwa akichezea Philadelphia Union ya Marekani- hao ni kwa upande wa wachezaji wapya.
    Nizar
    Wachezaji wa zamani ambao hadi sasa wamekwishafika Jangwani ni Juma Seif ‘Kijiko’, ambaye kulikuwa kuna tetesi anakwenda Simba, Hamisi Kiiza, Kenneth Asamoah, Yaw Berko, Shamte Ally, Jerry Tegete, Stefano Mwasyika, Godfrey Taita, Athumani Iddi ‘Chuji’, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Idrisa Senga, Omega Seme na Ibrahim Job.
    Yanga imeanza mazoezi jana kujiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, inayotarajiwa kuanza Julai 14 hadi 29, ikishirikisha na timu  nyingine mbili za Tanzania, Simba SC mabingwa wa Ligi Kuu na Azam FC washindi wa pili.
    Yanga ndio mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, baada ya mwaka jana kuifunga Simba SC kwenye fainali bao 1-0, mfungaji Kenneth Asamoah. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARTHEZ AANZA MAZOEZI RASMI YANGA JIONI HII Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top