![]() |
Mrwanda |
MAKAMU Mwenyekiti wa mabingwa wa Tanzania, Simba SC, Geoffrey
Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba wamekamilisha usajili wao kwa kukinasa kifaa kimoja
kikali ambacho Yanga walikuwa wanakiwania, ila wakaishia kunawa.
Ingawa Kaburu hakutaka kutaja jina la mchezaji huyo, lakini
uchunguzi wa BIN ZUBEIRY umebaini kwamba, mchezaji mwenyewe ni mshambuliaji
wa Dong Tam Long An ya Vietnam, Danny Davis Mrwanda ambaye kweli Yanga walikuwa
wanamtaka wakashindwana.
BIN ZUBEIRY inajua Mrwanda aliyewahi kuchezea Simba kabla ya
kwenda ughaibuni, atasaini Simba SC wakati wowote kwa sababu mazungumzo baina
ya pande hizo mbili yanaendelea vizuri.
Mkataba ambao atasaini Mrwanda ni ambao utamruhusu kuondoka
wakati wowote atakapopata timu nje ya Tanzania.
Pamoja na ishu ya Mrwanda, Kaburu alisema kwamba mchezaji
anayefunga usajili wa Simba ni beki wa kati wa kigeni, ambaye bado wanafuatilia
uwezo wake ili kujiridhisha.
Lakini Kaburu amesema mahitaji yote ya Simba yametimia, kwa
kusajili winga Kiggi Makassy, washambuliaji Abdallah Juma, Mrwanda, viungo Ibrahim
Jeba, Patrick
Mbivayanga, Salim Kinje, Mussa Mudde, beki wa kushoto, Paul Ngalema
na kupandisha wachezaji watatu wa U-20.
Aidha, Kaburu alisema ili kuboresha zaidi kikosi,
wanafikiria kusajili beki wa kulia kwa sababu Nassor Masoud ‘Chollo’ ni
majeruhi wa muda mrefu na kuna uwezekano bahati ikamuangukia beki wa timu hiyo
aliyekuwa akicheza kwa mkopo Villa Squad, Haruna Shamte.
![]() |
Kaburu |
“Shamte bado kijana mdogo, amecheza msimu mzima Villa Squad
na amecheza vizuri, tutamuita mwalimu (Mserbia Milovan Cirkovick) amuone,
akiridhika naye, atasajiliwa, Amri Kiemba tumemrudisha tayari, kwa sababu
mwalimu alimuona akaridhika naye”alisema Kaburu.
Lakini pia Kaburu alisema kwamba wanasaka makipa wawili, kwa
sababu kipa wao wa pili Ally Mustafa ‘Barthez’ amesaini Yanga na kipa wa tatu
William Mweta ni majeruhi wa muda mrefu pia.
Wakati huo huo: Kiggi Makassy ameripoti rasmi kazini, kwa
mwajiri wake mpya Simba SC na kuanza mazoezi leo asubuhi. “Kiggi ameanza mazoezi
rasmi leo,”alisema Kaburu kuhusu kiungo huyo waliyemuiba kwa watani wao wa jadi,
Yanga SC.
0 comments:
Post a Comment