• HABARI MPYA

    Wednesday, June 20, 2012

    KONGAMANO LA MICHEZO NA AMANI KESHO UBUNGO


    Thadeo, Mkurugenzi wa Michezo

    Na Princess Asia
    KONGAMANO linalohusu michezo na amani (National forum on sport for development and peace) linatarajiwa kufanyika kesho mjini Dar es Salaam, BIN ZUBEIRY imeiapta hiyo.
    Kongamano hilo limeandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushirikiana na Taasisi ya Right to Play na British Council litafanyika kwa siku mbili kesho na keshokutwa, katika hoteli ya Blue Pearl, Ubungo, Dar es Salaam .
    Mkurugenzi wa Idara ya Michezo nchini, Leonard Thadeo amesema kongamano hilo litawashirika wadau mbalimbali wa michezo kutoka ndani na nje ya nchi.
    Amesema lengo la kongamano hilo ni kutoa fursa kwa wadau kubadilishana mawazo na kuelezana changamoto zinazoikabili sekta hiyo. Mbali na kubadilishana mawazo, wadau hao pia wataangalia sera ya michezo nchini na kutoa ushauri wa nini kifanyike ili kufikia malengo yaliyomo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KONGAMANO LA MICHEZO NA AMANI KESHO UBUNGO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top