Simba SC |
Na
Princess Asia
SIMBA SC imetoka sare ya bila kufungana na All Stars
ya Zanzibar katika mchezo wa kirafiki jana usiku uliofanyika Uwanja wa Amaan,
Zanzibar kujiandaa na mechi dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC.
Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake ya
pambano dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC, Oktoba 3, mwaka huu, ikifanya
mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Kiislam, Kwerekwe, visiwani Zanzibar na kambi
yao ipo Chukwani.
Morali ya kambi ipo juu na wachezaji wote wako fiti,
wakijifua kwa shauku kubwa ili kumvutia kocha Mserbia, Milovan Cirkovick awape
nafasi ya kucheza Oktoba 3, kuanzia sa 1:00 usiku.
Simba ilirejea jana Zanzibar, baada ya juzi kuendeleza
wimbi lake la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kwa kuichapa Prisons
ya Mbeya iliyorejea Ligi Kuu msimu huu mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Mabao ya Simba yalitiwa kimiani na Felix Mumba Sunzu
na Mrisho Ngassa, ambaye hilo ni bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ndani ya
mechi nne na la pili jumla tangu ajiunge na timu hiyo katika mechi saba
alizocheza, wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri.
Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 12 na
kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi Azam FC pointi mbili katika nafasi ya
pili, ingawa timu zote zimecheza mechi sawa, nne.
0 comments:
Post a Comment