• HABARI MPYA

    Saturday, October 06, 2012

    BAHANUZI AMTEGUA BEGA KAPOMBE, KUWAKOSA OLJORO KESHO, NGASSA MALARIA IMEPANDA

    Bahanuzi nyuma ya Kapombe

    Na Princess Asia
    MABINGWA wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba SC kesho katika mchezo wao dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha watawakosa wachezaji wao wanne, wakiwemo beki Shomary Kapombe aliyeumizwa na mshambuliaji Said Bahanuzi wa Yanga Jumatano na Mrisho Ngassa, ambaye ana Malaria.   
    Ofisa Habari wa Simba SC, Ezekiel Kamwaga amesema leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu hiyo Mtaa wa Msimbazi kwamba, mbali na nyota hao wawili, wengine watakaokosekana kwenye mechi ya kesho ni mabeki Amir Maftahi anayetumikia adhabu ya kadi na Haruna Shamte, ambaye pia ni majeruhi.
    Kamwaga alisema kwamba Kapombe aliumizwa na mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanuzi Jumatano katika mechi baina ya watani hao wa jadi wa soka ya Tanzania, iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya 1-1.
    Kuhusu Ngassa, Kamwaga alisema kwamba baada ya mechi hiyo ya Jumatano, naye amepata Malaria, ambayo itamuweka nje ya Uwanja kesho, wakati Haruna aliumia mazoezini, timu hiyo ilipokuwa kambini Zanzibar ikijiandaa na mechi ya Yanga.
    Lakini Kamwaga alisema pamoja na kuwakosa nyota hao, anaamini wachezaji wengine watakaochukua nafasi zao watafanya vizuri. Kumbuka Emmanuel Okwi amemaliza adhabu na kesho anaweza kuiongoza Simba kwenye mechi hiyo.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BAHANUZI AMTEGUA BEGA KAPOMBE, KUWAKOSA OLJORO KESHO, NGASSA MALARIA IMEPANDA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top