Felix Sunzu wa Simba akiwa chini ya ulinzi wa mabeki wa Yanga, Nadoir Haroub 'Cannavaro' aliye karibu na msaada wa Oscar Joshua nyuma yake |
Na Prince Akbar
REFA Mathew Akrama
kutoka Mwanza ndiye atakayechezesha mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, baina ya wapinzani wa jadi nchini, Yanga na Simba itakayochezwa
keshokutwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura ameiambia BIN
ZUBEIRY kwamba katika mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu itakayoanza saa 1:00
usiku na kurushwa moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini,
Akrama atasaidiwa na Samuel Mpenzu kutoka Arusha na Ephrony Ndissa wa Dar es
Salaam wakati refa wa mezani atakuwa Oden Mbaga pia wa Dar es Salaam.
Amesema tiketi kwa
ajili ya mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya
wapinzani wa jadi nchini, Yanga na Simba itakayochezwa keshokutwa Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam, zitaanza kuuzwa kesho kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es
Salaam.
Alivitaja vituo
vitakavyotumika kuuza tiketi hizo kuanzia saa 4 asubuhi ni Shule ya Sekondari
Benjamin Mkapa, Uwanja wa Taifa, Kituo cha Mafuta OilCom Ubungo, Mgahawa wa
Steers ulioko Mtaa wa Ohio/Samora, Dar Live Mbagala na Kituo cha Mafuta
Buguruni.
Alikumbushia viingilio,
cha chini kwenye mechi hiyo ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo
ni 19,648 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.
Watazamaji watakaoketi kwenye viti vya rangi ya bluu ambavyo ni 17,045 watalipa
sh. 7,000 kwa tiketi moja.
Sh. 10,000 ni kwa viti
vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 wakati VIP C inayochukua watazamaji
4,060 itakuwa sh. 15,000. Kwa upande wa VIP B tiketi ni sh. 20,000 na VIP A
yenye watazamaji 748 tu kiingilio kitakuwa sh. 30,000.
0 comments:
Post a Comment