• HABARI MPYA

    Friday, March 02, 2012

    FERGUSON ANA IMANI SANA NA DE GEA


    KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema kwamba angepedna kipa David de Gea kuimarika haraka na kumudu kuendana na aina ya mchezo wa Ligi Kuu ya England.
    De Gea amekuwa akipambana ili kumudu kucheza kwa kutumia nguvu kama inavyotakuwa katika soka ya English gtangu atue klabu hiyo kwa dau la pauni Milioni 18 msimu huu, akitokea Atletico Madrid ya Hispania.
    Pia Sir Alex, anaamini kipa huyo mwenye umri wa miaka 21 ana dalili zote za kipaji cha kipa mzuri katika vidole vyake na anaweza kuwa maarufu baadaye Old Trafford.
    "Kijana amejaaliwa kipaji. Yuko vizuri, lakini amekuwa na wakati mgumu wa kumudu kuendana na mchezo wa hapa," alisema Mscotland huyo.
    "Ni suala la kujiendeleza. Anafanya kazi kubwa gym. "Ikiwa ataimarika kama jiwe, bila kupoteza wepswi wake na kasi, itakuwa babu kubwa kwake."
    De Gea, ambaye mwanzoni alikuwa maarufu kwa kuvurunda, ameanza kuimarika siku za klaribuni baada ya kusota benchi kwa siku kadhaa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FERGUSON ANA IMANI SANA NA DE GEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top