• HABARI MPYA

    Friday, March 02, 2012

    BEKI YANGA AKWAMA ULAYA


    BEKI ngongoti Mkenya, aliyewahi kucheza Yanga, Joseph Shikokoti anatarajiwa kurejea kwao kesho baada ya kufeli majaribio katika klabu ya Gandzasar FC ya Armenia.
    bongostaz imepata habari za ndani kwamba Nahodha huyo wa Tusker ya Kenya, alishindwa kumvutia kocha wa Gandzasar FC katika mchezo wa kirafiki aliopewa kama majaribio.
    "Shikokoti ni mchezaji mzuri, lakini anafanya makosa mengina haendani na mfumo wetu wa uchezaji", alisema Mr. Khashmanyan, kocha wa Gandzasar.
    "Tulimpa Shikokoti nafasi ya ajabu, lakini kwa bahati mbaya, mambo hayakwenda vizuri. Ilikuwa ni uzofu mzuri kwake na tunamtakia kila la heri katika maisha yake ya soka", alisema Ken Joseph Msemaji wa ETSM, wakala wa michezo anayesihi London ambaye alimfanyia mpango huo mchezaji huyo.
    Shikokoti amekuwa Armenia kwa mwezi na atajiunga tena na Tusker atakaporejea.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI YANGA AKWAMA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top