• HABARI MPYA

    Friday, March 02, 2012

    SUB NNE BAADA YA DAKIKA 90, KITAELEWEKA JUMAMOSI


    SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA) kupitia bodi yake ya sheria, (IFAB), Jumamosi itaamua kama timu zitakuwa zikiruhusiwa kufanya mabadilikio ya wachezaji wanne katika muda wa nyongeza sambamba na mustakabali wa mstari unaogawa goli na Waislamu kucheza wamefunika vichwa.
    Mkutano wa 126 wa IFAB mjini Bagshot, Kusini Magharibi mwa London, pia utazungumzia adhabu kali zaidi, iliyopewa jina "triple punishment" ambayo itamhusu mchezaji ambaye atazuia kwa makusudi mpira unaoelekea kutinga nyavuni, kwamba pamoja na adhabu ya penalti na kadi nyekundu, pia afungiwe.
    IFAB itasikiliza pendekezo la kuongeza idadi ya wachezaji wa kutokea benchi kutoka watatu hadi wanne mchezo unapofika kwenye dakika 120 kwamba itaswaidia kuongeza ladha ya mchezo na kupunguza majeruhi.
    Bodi hiyo pia itapitia wazo la kutumia teknolojia golini, jambo ambalo limekuwa mjadala mkubwa kwa kafribu muongo wote huu.
    FIFA imesema kwamba uamuzi wa mwisho kuhusu kutumia teknolonjia golini utachukuliwa katika mkutano mwingine wa  IFAB, unaotarajiwa kufanyika Julai 2, siku moja baada ya fainali ya michuano ya Euro 2012, mjini Kiev.
    IFAB pia itatafakari wazo la kutumia marefa watano, kwa kuongeza refa mmoja nyuma ya goli kuwasaidia marefa watatu wanaotumika kwa sasa.
    Naye Prince Ali wa Jordan, Mjumbe mdogo zaidi kwa umri wa katika Kamati ya Utendaji ya FIFA, atawasilisha ombi la kutaka wacghezaji wa kike wa kiislamu waruhusiwe kuvaa hijab, ikiwa ni miakia mitano baada ya vazi hilo kupigwa marufuku kwenye soka kwa sababu za kiusalama.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUB NNE BAADA YA DAKIKA 90, KITAELEWEKA JUMAMOSI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top