KLABU ya Manchester City imempa muda zaidi Carlos Tevez
kabla ya kurejea kwenye kikosi cha kwanza cha klabu hiyo, kwanza afanye programu
maalum ya kujieka fiti, baada ya Muargentina huyo kushindwa kufanya vizuri
alipopewa dakika 45 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa milango imefungwa.
Mshambuliaji huyo ambaye, ambaye hajachezea vinara hao wa
Ligi Kuu tangu agome kupasha misuli moto aingie kuichezea City ikiwa nyuma 2-0 mbele
ya Bayern Munich Septemba, mwaka jana katika mechi ya Ligi ya Mabingwa,
alionekana mchovu aklicheza dakika 45 za kwanza mbele ya Ofisa Utawala wa soka,
Brian Marwood na Mkurugenzi wa Maendeleo, Patrick Vieira katika ushindi wa 3-1
dhidi ya Preston.
Akiwa nje ya klabu kwa miezi kadhaa, amepumzika nyumbani
kwao Argentina, bongostaz inatambua kwamba Tevez anatakiwa kupewa muda zaidi
ili kujiweka fiti kwa kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Bolton katika
michuano ya Manchester Senior Cup Jumanne.
City awali ilitumai kumjumuisha mchezaji huyo mwenye umri wa
miaka 28 katika kikosi kitakachocheza mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Swansea, Machi
11, lakini kutokana na mshambuliaji huyo kucheza ovyo, klabu hiyo sasa imemsogezea
mbele muda wa kurejea uwanjani hadi kwenye mechi dhidi ya Chelsea, Machi 19.
Tevez alisema atahitaji wiki mbili tu za kujifua kabla ya
kuanz akazi rasmi.
0 comments:
Post a Comment