• HABARI MPYA

    Friday, March 02, 2012

    RAUL AONGEZEWA MAISHA SCHALKE


    KLABU ya Schalke imempa ofa Nahodha wa zamani wa Real Madrid, Raul Gonzalez kuongeza mkataba wa kuichezea timu hiyo ya Bundesliga.
    Meneja Mkuu wa Schalke, Horst Heldt alisema jana kwamba wamempa Raul ofa ya kuongeza mkataba, ambao unamalizika mwisoni mwa msimu, taarifa ambayo ametumiwa mwakilishi wake nchini Hispania, Gines Carvajal.
    Mkongwe huyo mwenyr umri wa miaka 34, Raul amefunga mabao 25 katika mechi 56 za ligi akiwa na jezi ya Schalke tangu ajiunge nayo mwaka 2010 akitokea Real Madrid. Amefunga mabao 33 katika michuano yote akiwa na klabu hiyo na Ujerumani, yakiwemo 14 msimu huu.
    Nahodha huyo wa zamani wan Hispania, aliiwezesha klabu hiyo kutwaa Kombe la Ligi Ujerumani katika msimu wake wa kwanza Schalke, mwaka jana.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAUL AONGEZEWA MAISHA SCHALKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top