• HABARI MPYA

    Sunday, May 20, 2012

    DAVIED SEAMAN AANGUKIA KWENYE UVUVI


    BAADA ya kucheza soka kwa miaka 22 mlinda mlango wa zamani wa Arsenal David Seaman aliamua kustaafu akiwa na umri wa miaka 40 na kuamua kutumia muda wake kwa ajili ya kufanya shughuli za uvuvi.
    Lakini mwaka 2009, mke wake, Seaman, Debbie, alitangaza kuwa mumu wake huyo ambaye sasa wameachana alikuwa akimuaga kuwa anakwenda kuvua na kuwinda usiku, lakini alijiingiza katika kufanya mapenzi kisisiri.
    Seaman mwenye umri wa miaka 45, aliachana na mke wake aliyezaa naye watoto wawili Februari mwaka 2009, kutokana na tabia mbaya ya mlinda mlango huyo kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.
    Debbie Seaman mwenye umri wa miaka 47, kwa mara ya kwanza aligundua kama mumewe ‘anacheza mechi za ugenini’ baada ya kukuta picha ya mwanamke kwenye simu Seaman iliyotumwa kwa njia ya ujumbe.
    Mke huyo alimuuliza mumewe na huyo ambaye walidumu kwa miaka 10 kwenye ndoa yao na kumjibu kuwa ilikuwa picha ya mwanamke mmoja wa anayeishi Mjini Birmingham na wala haina maana yoyote akimtaka apuuzie.
    Mwanamke huyo hakutaka kuvunja ndoa yake na kuamua kuendelea kukaa na mumewe ingawa alipofuatilia juu ya simu hiyo aligundua kuwa Seaman alianza kuwasiliana na mwanamke huyo tangua mwaka 2005 wakati huo wao walioana mwaka 1998.
    Pamoja na mwanamke huyo ambaye Debbie aligundua kuwa alikuwa ameshafanya mapenzi na mumewe mara nyingi, pia mumewe huyo alikuwa na mawasiliano kwa njia ya ujumbe na mwanamke mwingine kwa muda wa miezi mitatu.
    Lakini mlinda mlango huyo aliendelea kumsisitizia mke wake kuwa hakuna jambo lolote linaloendelea yeye na wanawake hao na mda si mrefu ataacha kuwasiliana nao, ila mkewe hakuwa akimwamini tena kutokana kuwa na mahusiano na wanawake wawili nje ya ndoa yake hiyo.
    Fabruari mwaka 2009, Seaman aliondoka nyumbani kwake Hertfordshire muda wa jioni bila kuacha taarifa yoyote, alipopigiwa simu hakupokea hadi saa 11 alfajiri na kusema kuwa alikuwa hataki kuoana na mkewe huyo kwa hiyo hana mpango wa kurejea nyumbani kwake tena.
    Baadaye alirejea nyumbani akiwa na mwanake mwingine aitwaye Frankie Poultney dansa wa kwenye barafu mwenye umri wa miaka 35 na mkewe alisikia taarifa hiyo kupitia vyombo vya habari kwamba mumewe ana mpenzi mwingine.
    Seaman na Debbie walianza mahusiano baada ya mlinda mlango huyo kuachana na mke wake wa kwanza aliyeishi naye kwa miaka 10 pia aliyekuwa akiitwa Sandra.
    Nyota huyo aliyekuwa amepanga kujihusisha kwenye uvuvi na kucheza gofu baada ya kuacha soka mwaka 2004, mwaka 2006 alionekana kwenye kipindi kimoja cha Televisheni ya ITV akiwa kwenye kipindi cha ‘live’ cha kudansi kwenye barafu akiwa na mshirikia wake kwenye mchezo huo Pam O’Connor.
    Mpenzi wake mpya Poultney na yeye alionekana kwenye kipindi hicho kwa mara ya kwanza mwaka uliyofuata akicheza na mchezaji wa zamani wa Manchester United Lee Sharpe.
    David Andrew Seaman, alizaliwa Septemba 19 mwaka 1963, Rotherham, Kusini mwa Mji wa Yorkshire nchini England, amecheza klabu mbalimbali lakini muda mwingi ameutumia akiwa Arsenal kabla ya kustaafu Januari 13 mwaka 2004, kutoka na maumivu ya bega yasiyopona,
    Wakati akiwa Arsenal alifanikiwa kutwaa mataji mbalimbali, mataji mataji matatu ya Ligi Kuu ya England 1991, 1998, 2002, Kombe la FA mara nne mwaka 1993, 1998, 2002, 2003), Kombe la Ligi mwaka 1993 na Kombe la Washindi la barani Ulaya mwaka 1994.
    Kwa kipidni chake cha soka alicheza kwenye timu ya Taifa kwenye fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1998 na 2002, Mataifa ya Ulaya mwaka 96 na Euro 2000, alicheza jumla ya mechi 75, akiwa ni mlinda mlango wapili wa England kucheza mechi nyingi baada ya Peter Shilton.
    Seaman alionyesha kiwango kizuri kwenye timu ya Taifa ya England wakati wa michuano ya Mataifa ya Ulaya mwaka 1996 na kwa upande wa Arsenal kipindi chake kizuri kilikuwa ni mwaka ni wakati wa Kombe la UEFA na Ligi Kuu ya England katika msimu wa mwaka 2002–03.
    Na vipindi vibaya kwa mlinda mlango huyo ilikuwa ni mwaka 1995 wakati wa Kombe la UEFA kwa klabu yake ya Arsenal alipofungwa bao la mbali kwenye fainali na Nayim na fainali za Kombe la Dunia mwaka 2002 Ronaldinho alimtungua kwa mpira wa mbali wa adhabu kwenye hatua ya robo fainali dhidi ya Brazil.
    Seaman alikulia Mjini Rotherham na kusoma shule ya Kimberworth Comprehensive na kuanza kucheza soka lake kwenye klabu ya Leeds United, lakini klabu yake ilimuunga mkopno kocha Eddie Gray, ambaye alikuwa hamtaki Seaman, ingawa mlinda mlango huyo alikuwa akimpenda Gray tangu akiwa mchezaji.
    Seaman aliuzwa kwenye timu ya Daraja la Nne iitwayo Peterborough United Agosti mwaka 1982 kwa ada ya pauni 4,000 na kuanza kujitengenezea jina na baada ya miaka miwili Oktoba mwaka 1984, alijiunga na timu ya Daraja la Pili ya Birmingham City kwa pauni 100,000.
    Klabu hiyo ilipanda Ligi Daraja la Kwanza lakini mwaka uliyofuata ikashuka tena na
    Agosti mwaka 1986, Queens Park Rangers walilipa pauni 225,000 kwa ajili ya huduama ya Seaman na kucheza klabu hiyo iliyokuwa uwanja wenye nyasi za plastiki.
    Mwaka 1990, kabla ya mfumo wa sasa wa usajili England kulikuwa na nafasi ya kusajili wiki chache kabla ya kumalizika kwa msimu, hivyo Arsenal ambao walikuwa ni mabingwa wa Ligi hiyo mwaka 1989, walitaka kumsajili Seaman.
    Mpango huo ulitaka kumuhusisha mlinda mlango wa Arsenal John Lukic, ambaye alitakiwa kwenda QPR kwa mkopo ili kubadilishana na Seaman ila Lukic alikataa na dili likavunjika bila usajili huo kufanikiwa.
    Msimu uliyofuata kocha wa Arsenal wakati huo George Graham, alirejea kwenye klabu hiyo ya QPR na pauni milioni 1.3 na kumsajili Seaman aliyeweka rekoodi ya mlinda mlango aliyesajiliwa kwa bei kubwa na kumuacha mlinda mlango wa Arsenal Lukic aliyekuwa na mashabiki wengi Gunners kujiunga Leeds.
    Akiwa Arsenal Seaman alipata mafanikio makubwa na kutwa mataji mengi, ikiwa ni pamoja na kucheza msimu wa mwaka 1990–91 na kuruhusu mabao 18 tu katika mechi 38 alizocheza na kutetea taji lao na baada ya Terry Venables kupewa kibarua cha kuinoa England alimuona Seaman kama chaguo lake la kwanza na mlinda mlango alibakia kwenye kikosi hicho hadi mwaka 2002.
    Mwaka 1995, George Graham alifukuzwa na Arsenal walikaribia kutetea Kombe lao la UEFA, huku Seaman akionekana kama mchawi wa kudaka mikwaju ya penalti baada ya kunasa penalti ya Attilio Lombardo wakati wa hatua ya nusu fainali na Gunners kuwatoa Sampdoria.
    Lakini walifungwa kwenye mchezo wa fainali katika muda wa nyongeza baada ya mchezaji wa Real Zaragoza Nayim, kufunga bao la umbali wa yadi 45 wakati Seaman akiwa ametoka kidogo kwenye mstari wa lango lae.
    Hata alipotua Arsene Wenger Agosti mwaka 1996 kuinoa Arsenal, Seaman aliendelea kupewa nafasi na msimu wa mwaka 1998–99, alicheza mechi zote 38 na kuruhusu mabao 17 na kwenye nusu fainali ya Kombe la FA, Arsenal walitolewa nje na  Manchester United, huku wakifungwa penalti kwenye fainali ya Kombe la UEFA dhidi ya Galatasaray mwaka 2000 baada ya kutoka sare ya 0-0.
    Seaman alishinda mataji mawili kwa mwaka 2002, Kombe la FA na lile la Ligi Kuu ya England, pamoja kumaliza vibaya soka lake kwa upande wa timu ya Taifa kutoka na umri kuwa mkubwa, aliokoa shambulizi la kukumbukwa msimu wa mwaka 2002–03 katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA dhidi ya Sheffield United.
    Mchezaji wa Sheffield Paul Peschisolido alipiga kichwa akiwa ndani ya kiboksi kidogo, huku Seaman akiwa ametoka langoni kwenda kuokoa mpira wa kona lakini aliruka na kuugusa mpira huo ambao ulidondoka eneo na hatari na mchezaji mwingine wa Sheffield akapiga shuti lililokwenda juu, huku zikiwa zimesalia dakika chache kabla mpira haujaisha na Arsenal kushinda bao 1-0.
    Wakati wa mechi hiyo ya nusu fainali mlinda mlango wa Manchester United wakati huo Peter Schmeichel, ndiye alikuwa mchambuzi wa mechi hiyo kwenye kituo cha Televisheni cha BBC na kusifu akisema: “Seaman amefanya kazi ambayo sijawahi kuona mlinda mlango yoyote akifanya.”
    Seaman amekaa langoni mwa Arsenal kwa muda mrefu zaidi na kuwa mchezaji wa pili kucheza mechi nyingi baada ya Ray Parlour, mlinda mlango huyo amecheza mechi 325 na Juni mwaka 2008 alitajwa kama mchezaji namba saba kati ya wachezaji 50 wa Gunners.
    Alichwa kwenye klabu hiyo ya Arsenal mwaka 2003 na kujiunga Manchester City chini ya kocha Kevin Keegan, lakini hakuweza kucheza kwa muda mrefu kwenye klabu hiyo baada ya kusumbuliwa na majeruhi yasiyopona na Januari mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 40 alitangaza kuacha soka.
    Seaman alianza kucheza kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya Taifa mwaka 1988, baada ya kuitwa na kocha Bobby Robson na Novemba mwaka huo alicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Saudi Arabia ikiwa ni mchezo wa kirafiki.
    Alikuw amechaguliwa kama mlinda mlango namba tatu akiwa na akina Peter Shilton na Chris Woods wakati wa fainali za Kombe la Dunia mwaka 1990.

    WASIFU WAKE
    JINA: David Andrew Seaman
    KUZALIWA: Septemba 19 mwaka 1963 (48)
    ALIPOZALIWA: Rotherham, England
    UREFU: Futi 6 inchi 3
    TIMU ALIZOCHEZEA:
    1981–1982      Leeds United (Academy)
    1982–1984      Peterborough United (mechi 91)
    1984–1986      Birmingham City (mechi 75)
    1986–1990      Queens Park Rangers (mechi 141)
    1990–2003      Arsenal (mechi 405)
    2003–2004      Manchester City (mechi 19)
    JUMLA:          Mechi 731
    (Tangu 1988 hadi 2002 aliichezea England mechi 75)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DAVIED SEAMAN AANGUKIA KWENYE UVUVI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top