Patrice Evra-ana imani
BEKI na nahodha wa klabu ya Manchester
United Patrice Evra bado ana imani klabu yake inaweza kuondoka na ushindi wa
Ligi kuu.
United, ikiwa katika nafasi ya pili kwa
tofauti ya magoli tu, inahitaji kuiona City ikijikwaa dhidi ya QPR au uwezekano
wa kuimiminia Sunderland mabao yasiyopungua tisa ili kuiondoa City kileleni kwa
hio tofauti ya magoli manane.
Evra anasema, huenda watu watadhani
nimechanganyikiwa, lakini ni imani niliyo nayo.
"naelewa kua hatma ya matokeo haimo
mikononi mwetu. Lakini ikiwa tunataka kubaki na imani ya miujiza lazima
tuishinde Sunderland."
0 comments:
Post a Comment