• HABARI MPYA

    Tuesday, May 22, 2012

    KUMEKUCHA MISS DAR INTERCOLLEGE 2012


    Dina Ismail , Mratibu
    WAREMBO watakaoshiriki shindano la Miss Dar Inter College 2012, kesho  wataanza kujinoa  kwenye hoteli ya Lamada, jijini Dar es Salaam ikiwa ni katika maandalizi ya shindano lao litakalofanyika baadaye mwezi ujao.
    Mratibu wa shindano hilo Dina Ismail Mkingiye ameiambia BIN ZUBEIRY mchana wa leo kwamba  warembo hao watatoka vyuo vya  Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time, pamoja na  Ustawi wa Jamii.
    “Kesho  tutaanza mazoezi yetu pale Lamada ambapo warembo kutoka vyuo vinne wataanza kujinoa…wiki ijayo huenda tukaongeza washiriki wengine ambao watatoa chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) ambao wanafanya shindano lao mwishoni mwa wiki hii,”alisema.
    Alisema kuwa warembo hao watakuwa chini ya ukufunzi wa  mrembo aliyepata kushiriki shindano hilo, Rose John, huku kwa upande wa shoo watanolewa na Bob Rich.
    Dina aliwataja wadhamini waliojitokeza mpaka sasa ni pamoja na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, na  Dodoma Wine, huku akiomba makampuni mengine kujitokeza kudhamini shindano hilo litakalofanyika mwezi ujao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KUMEKUCHA MISS DAR INTERCOLLEGE 2012 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top