• HABARI MPYA

    Friday, December 07, 2012

    SUNZU ATUPIWA VIRAGO SIMBA SC

    Sunzu akitibiwa na daktari wa Simba, Dk Cossmas Kapinga katika moja ya mechi za Ligi kuu mzunguko wa kwanza msimu huu. 

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Zambia, Felix Mumba Sunzu Jr. ametemwa kwenye kikosi cha Simba SC kutokana na kuomba yeye mwenyewe na uongozi wa klabu hiyo kuridhia.
    Habari za ndani kutoka Simba SC, zimesema kwamba Sunzu alifika Dar es Salaam na kuzungumza na viongozi wa klabu hiyo, akiomba aachwe kwani hawezi kucheza kwa sasa kutokana na matatizo ya kiafya yanayomkabili.
    “Sunzu bwana amekuja mwenyewe kuomba na sisi baada ya kuona hali yake, kwa kweli kibinadamu tumemkubalia aende,”kilisema chanzo chetu kutoka Simba SC.
    Sunzu alisajiliwa Simba SC Julai 25 mwaka jana, akitokea El Hilal ya Sudan akisaini mkataba wa miaka miwili kwa dola za Kimarekani 35,000 na mshahara wa dola 3,000.
    Kutemwa kwa Sunzu kunafanya idadi ya wachezaji wa kigeni waliotemwa Simba kufika watatu, baada ya awali kutemwa beki Paschal Ochieng kutoka Kenya na mshambuliaji Daniel Akuffo kutoka Ghana.
    Simba inamrejesha kikosini Mussa Mudde na kusaini Waganda wapya wawili, kipa Hamza Muwonge na mshambuliaji Brian Umony, ambao wataungana na Mganda mwenzao kwenye klabu hiyo, Emmanuel Okwi kufanya idadi ya wageni watano kwa mujibu wa kanuni za Bara.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SUNZU ATUPIWA VIRAGO SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top