![]() |
Miembeni itaing'oa Tusker leo? |
Na Mahmoud Zubeiry
TUSKER FC
inashuka dimbani leo usiku kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar kumenyana na
Miembeni katika Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Mapinduzi.
Mchezo huo,
unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua, kwani kwa sasa Miembeni ndiyo timu
inayoiwakilisha vema Zanzibar katika mashindano haya na inaungwa mkono na Wazanzibari
wengi.
Kocha wa
Miembeni Salum Bausi amesema hawahofii Tusker na leo atawaonyesha kwamba mpira
ni zaidi ya nguvu.
Nahodha wa
Tusker, Joseph Shikokoti amesema kwamba haoni timu ya kuwazuia kutwaa Kombe la
Mapinduzi.
Shikokoti
aliyewahi kuchezea Yanga alisema kwamba anafahamu Simba na Azam ni wazuri na
anajua mojawapo watakutana nayo fainali, lakini amesistiza hakuna kati yao
inayoweza kuwazuia wasitwae Kombe.
“Hili Kombe
letu, tumeona uwezo wa timu zote, hata Simba na Azam ni wazuri, lakini
tutawafunga wote tukikutana nao, hawana uwezo wa kutuzuia,”alisema Shikokoti.
Nusu Fainali
ya pili itachezwa kesho kati ya Simba SC na Azam FC.