• HABARI MPYA

    Wednesday, May 15, 2013

    BRIAN KIDD AANZA VEMA MAN CITY AKIRITHI MIKOBA YA MANCINI KWA KUIFUMUA TIMU YA MWAMEJA 2-0


    IMEWEKWA MEI 15, 2013 SAA 7: 54 USIKU
    SIKU moja baada ya Roberto Mancini kutupiwa virago Manchester City, timu hiyo imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini Uwanja wa Madejski dhidi ya wenyeji Reading, klabu ambayo amewahi kuchezea kipa Mtanzania, Mwameja Mohamed ikiwa Daraja la Tatu. 
    Ikiwa chini ya aliyekuwa msaidizi wa Mancini, Brian Kidd, Man City leo ilipata mabao yake kupitia kwa Aguero dakika ya 40 na Dzeko dakika ya 88.
    Kikosi cha City, leo kilikuwa; Hart, Richards, Toure/Maicon dk15, Lescott, Clichy, Toure, Barry/Garcia dk58, Milner, Silva, Tevez na Aguero/Dzeko dk62. 
    Reading: McCarthy, Gunter, Morrison, Mariappa, Kelly, Karacan, Guthrie, McCleary, McAnuff/Blackman dk69, Robson-Kanu, Pogrebnyak/Le Fondre dk62. 

    First of all: Brian Kidd led City to a win in his first game as caretaker manager
    Mwanzo mzuri: Brian Kidd ameiongoza City kushinda mechi ya kwanza chini yake kama kocha wa muda
    One ahead: Aguero put City 1-0 up in the first half after a lovely team move
    Aguero aliifungia bao la kwanza City.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BRIAN KIDD AANZA VEMA MAN CITY AKIRITHI MIKOBA YA MANCINI KWA KUIFUMUA TIMU YA MWAMEJA 2-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top