IMEWEKWA AGOSTI 15, 2013 SAA 12:42 JIONI
KLABU ya Manchester United inaendelea kumfuatilia Cristiano Ronaldo baada ya makocha Phil Neville na Steve Round kumshuhudia nyota huyo wa zamani wa Old Trafford akiichezea Ureno jana usiku.
Neville na Round walikuwa kwenye Uwanja wa Algarve kumshuhudia Ronaldo akifunga bao la jioni kuinusuru kuzama mbele ya Uholanzi kwa kupata sare ya 1-1 ya Robin van Persie.
United imetunza jezi namba saba (7)zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya kuanza kwa msimu mpya kwa matumaini ya kutimiza ndoto za kumrejesha Ronaldo kutoka Real Madrid – miaka minne baada ya kutimkia Bernabeu kwa sau la rekodi ya dunia, Pauni Milioni 80.
Anatakiwa: Ronaldo aliifungia bao la kusawazisha Ureno katika sare ya 1-1 na Uholanzi jana
Jopo la makocha: David Moyes akizungumza na Neville na Round katika mchezo wa kumuaga Rio Ferdinand Ijumaa
Mustakabali wa mchezaji huyo umeendelea kuwa shakani Hispania, licha ya Rais wa Real, Florentino Perez kuhakikisha kwamba atasaini Mkataba mpya.
Na huku David Moyes na Mtendaji Mkuu mpya United, Ed Woodward wakiwa bado hawajasajili mchezaji yeyote tangu waanze kazi na tetesi zikizidi juu ya Wayne Rooney kuondoka, United inafahamu kwamba kumnasa Ronaldo watawapa mtikisiko wapinzani wao wote ndani na nje ya Uwanja.
Ronaldo akirekebisha nywele zake jana
Mshindi: Ronaldo akishangilia dhidi ya FC Porto katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2009
Spesho Namba 7: Valencia amepokonywa jezi namba saba na sasa iko wazi baada ya kushindwa 'kuitendea haki' kama wachezaji waliomtangua