IMEWEKWA SEPTEMBA 6, 2013 SAA 3:11 ASUBUHI
KLABU ya Barcelona inamtaka kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois awe kipa wao namba moja msimu ujao na imeanza harakati za kumchukua.
BIN ZUBEIRY inafahamu wamemuweka juu ya kipa wa Borussia Moenchengladbach, anayepewa thamani kubwa Marc-Andre ter Stegen katika orodha ya makipa wanaotaka warithi mikoba ya Victor Valdes.
Huku Petr Cech akiwa hajaonyesha dalili za kuachia mikoba ya kipa namba moja Stamford Bridge, Mbelgiji huyo anaidakia kwa mkopo Atletico Madrid keeper na inafahamika anapenda kujiunga na vigogo wa Katalunya katika kusaka namba ya kudumu kikosi cha kwanza.
Kipa matawi ya juu: Thibaut Courtois ni miongoni mwa makipa bora duniani
Wakongwe: Lakini ikiwa Petr Cech (kulia) atabakia Chelsea, Courtois ataombwa kuchukua nafasi ya Victor Valdes
Gharama bado hazijawekwa wazi. Wakati thamani ya Ter Stegen ni kiasi cha Pauni Milioni 10, Chelsea inatarajiwa kuomba fedha mara ya tatu ya hizo ili kumuuza Courtois, ambaye amefanya vizuri katika misimu yake miwili ya awali Madrid.


.png)