• HABARI MPYA

    Sunday, February 16, 2014

    MESSI AWEKA REKODI MPYA HISPANIA BARCA IKIUA 6-0 LA LIGA

    MSHAMBULIAJI Leo Messi amewapashia misuli Manchester City kwa kuweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika historia ya soka ya Hispania, baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa Barcelona wa 6-0 dhidi ya Rayo Vallecano usiku huu. 
    Ushindi huo unaifanya Barca itimize pointi 57 baada ya kuchea mechi 23 La Liga na kupanda nafasi ya pili, nyuma ya Atletico Madrid yenye pointi 60, lakini imecheza mechi moja zaidi.
    Real Madrid ina pointi 57 pia katika nafasi ya tatu kutokana na kuzidiwa wastani wa mabao na Barca. 
    Dole tupu: Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi akishangilia baada ya kufunga dhidi ya Rayo Vallecano Uwanja wa Nou Camp leo
    Should have stayed on your line: Messi chips the ball over Rayo Vallecano's goalkeeper Ruban Martinez
    Messi akimtungua kipa wa Rayo Vallecano, Ruban Martinez

    Messi alifunga mabao yake dakika za 38 pasi ya Fabregas na dakika ya 68 pasi ya Sanchez,wakati mabao mengine yalifungwa na Adriano Correia dakika ya pili pasi ya Pedro, Sanchez dakika ya 53 pasi ya Messi, Pedro dakika ya 56 pasi ya Fàbregas na Neymar dakika ya 89 pasi ya Iniesta.
    Messi sasa ametimiza mabao 227 katika mechi 262 Hispania, akimpiku mshambuliaji wa zamani wa Real Madrid, Di Stefano aliyefunga mabao 227 katika mechi 329.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AWEKA REKODI MPYA HISPANIA BARCA IKIUA 6-0 LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top