• HABARI MPYA

    Saturday, July 05, 2014

    JAMES RODRIGUEZ AAGA KOMBE LA DUNIA MKONO KWENYE KIATU CHA DHAHABU

    NYOTA aliyeng’ara katika Kombe la Dunia Brazil, James Rodriguez anaondoka kwenye michuano hiyo baada ya timu yake kulala 2-1 mbele ya wenyeji, Brazil, lakini akiwa amenyoosha mkono kwenye kiatu cha dhahabu.
    Chipukizi huyo wa Monaco ya Ufaransa leo amefunga bao la sita katika mashindano hayo, akiendeleza utamaduni wake wa kufunga katika kila mechi tangu kuanza kwa michuano.
    Rodriguez pamoja na kuwekewa ulinzi mkali na mabeki wa Brazil leo, lakini alifanikiwa kuifungia timu yake bao la kufutia machozi kwa penalti dakika ya 80.
    Mkali kweli: James Rodriguez anaaga Kombe la Dunia akiwa anaongoza kufunga mabao

    WANAOWANIA KIATU CHA DHAHABU KOMBE LA DUNIA

    6 - James Rodriguez (Colombia)
    4 - Thomas Muller (Ujerumani), Lionel Messi (Argentina), Neymar (Brazil)
    3 - Karim Benzema (Ufaransa), Arjen Robben (Uholanzi), Robin van Persie (Uholanzi), Enner Valencia (Ecuador), Xherdan Shaqiri (Switzerland)
    (Maandishi yaliyolazwa nchi hizo zimetolewa Kombe la Dunia).
    Penalti hiyo ilitolewa na refa wa Hispania, Carlos Velasco Carballo baada ya kipa Julio Cesar kumkwatua Rodriguez wakati anaenda kufunga baada ya kufanikiwa kuibomoa ngome ya Brazil.
    Sasa anaongoza kwa mabao, huku wanaomfuatia Thomas Muller wa Ujerumani, Lionel Messi wa Argentina na Neymar wa Brazil kila mmoja akiwa na mabao manne.
    Karim Benzema wa Ufaransa, Arjen Robben, Robin van Persie wote wa Uholanzi, Enner Valencia wa Ecuador na Xherdan Shaqiri wa Uswisi, kila mmoja ana mabao matatu.
    Nyota huyo anayezitoa udenda klabu kubwa za Ulaya hivi sasa, anarejea nyumbani huku akiwaombea dua mbaya wanaomfuatia kwa mabao wasifunge tena, ili ajifariji kwa kiatu cha dhabau cha kombe la Dunia baada ya kushindwa kutimiza ndoto za kutwaa taji hilo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JAMES RODRIGUEZ AAGA KOMBE LA DUNIA MKONO KWENYE KIATU CHA DHAHABU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top