• HABARI MPYA

    Sunday, August 03, 2014

    AMBAVYO REFA DENNIS BATTE 'ASIVYO NA HAYA'

    Refa Mganda, Dennis Batte akitoka uwanjani huku akiona aibu baada ya 'kuiuma sana' Tanzania katika mchezo dhidi ya Msumbiji Uwanja wa Zimpeto jioni ya leo. Tanzania ilifungwa 2-1 na kutolewa katika hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco. Pamoja na kukataa bao zuri la kichwa la Said Mourad aliyeunganisha mpira wa adhabu wa Khamis Mcha 'Vialli', Batte aliwapigia filimbi za kuotea wachezaji wa Taifa Stars wakiwa hawajaotea.
    Beki Said Mourad akiwa ameruka juu kupiga mpira kichwa kuifungia Taifa Stars bao lililokataliwa na refa Dennis Batte

    Mourad akiwa amepiga mpira na kushoto kipa Dario Khan anatoka kufuata mpira, anapishana nao, huku Nadir Haroub 'Cannavaro' akimkwepa mlinda mlango huyo
    Mpira umetinga nyavuni, hili lingekuwa bao la kwanza katika mchezo huo ambalo lingewafanya Stars wacheze kwa mbinu za kulilinda, ili kushinda
    Dario Khan anaokota mpira nyavuni, huku chini refa Dennis Batte anakataa na wachezaji wa Tanzania, Cannavaro na Mbwana Samatta wanamlalamikia

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AMBAVYO REFA DENNIS BATTE 'ASIVYO NA HAYA' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top