• HABARI MPYA

    Sunday, August 03, 2014

    ARSENAL YAPIGWA KIDUDE NA MONACO KOMBE LA WENYEWE REFA AKIWANYIMA PENALTI NYEUPEEEE

    BAO pekee la Radamel Falcao jioni hii limeipa Monaco ushindi wa 1-0 dhidi ya Arsenal, katika Kombe la Emirates mjini London, lakini wenyeji wameondoka wakilia na refa Martin Atkinson kwa kuwanyima penalti ya wazi. 
    Upande wa pili wa sarafu, Arsenal watajilaumu wenyewe kwa kumruhusu mshambuliaji huyo mwenye thamani ya Pauni Milioni 53 kufunga kiulaini akiwa peke akiruka kuunganishia mpira nyavuni kwa kichwa.
    Refa Atkinson alitoa mpira nje licha ya Chubo Akpom kuangushwa ndani ya eneo la penalti na kipa wa Monaco, Daniel Subasic, maamuzi ambayo yalizua mzozo kidogo kabla ya mchezo kuendelea.

    Kiulaini: Mabeki wa Arsenal wakimtazama mshambuliaji wa Monaco, Falcao akiruka kufunga kwa kichwa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAPIGWA KIDUDE NA MONACO KOMBE LA WENYEWE REFA AKIWANYIMA PENALTI NYEUPEEEE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top