• HABARI MPYA

    Friday, August 22, 2014

    NANI KUWA MISS TEMEKE LEO? SHOO LINAPIGWA TCC NA BURUDANI KIBAO ZIKIONGOZWA NA MNYAMA TID

    Na Dina Ismail, DAR ES SALAAM
    NANI kati wa washiriki 17 ataibuka kuwa mshindi wa shindano la Redd's Miss Temeke 2014, linalofanyika kesho kwenye Ukumbi wa TCC Club Chang'ombe Dar es Salaam.
    Jumla ya warembo 17 kutoka vitongoji vya Mbagala, Kurasini na Chang;ombe watapanda jukwaani kuwania taji hilo, huku washindi wa tatu watapata nafasi ya kushiriki shindano la Miss Tanzania mwaka 2014.
    Akizungumza Dar es Salaa jana Mkurugenzi BMP Promotions, Benny Kisaka, alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yamekamilika kama yalivyopangwa.
    Washiriki wa Miss Temeke 2014, je nani kati yao atang'ara usiku wa leo?

    Kisaka alisema kuwa taji linaloshikiliwa na mrembo kutoka kanda ya kati, lakini mwaka huu Temeke imejizatiti kutoa si tu Miss Tanzania, mbali warembo watatu wa kwanza wa Taifa kutokana na viwango vya warembo wa mwaka huu.
    Alisema kuwa mbali ya shindano hilo kubwa, kulifanyika shindano dogo la awali lililoandaliwa na Michuzi Media la Miss Photogenic ambalo mshindi wake atazawadiwa kitita cha Sh. milioni 1 taslimu, shindano ambalo lililsimamiwa na jopo la wapiga picha wa kampuni hiyo ambao watamtangaza na kumpa zawadi mshindi siku ya shindano.
    Kisaka aliwataja Warembo wanaotarajiwa Subira Ally, Hellen Yughin, Catherine Alex, Dalina David, Winfrida Guntram, Salama Salehe, Grace John, Lilian Lothy, Amina Salim, Rebecca Mdamu, Sitti Mtemvu, Hellen Sule, Neema Mollel, Lucy Lewis, Esther Mnahi, Pauline Nkini na Patricia Ponsian ambao walikuwa chini ya ukufunzi wa Super Bokilo, Shadya Mohamed na Sweet Remmy.
    Alisema mkali wa bongofleva, Khalid Mohamed TID almaarufu kama Top in Dar, sanjari na Wanne Star, Makirikiri wa Tanzania, Young Suma, Super Bokilo na wasanii mbalimbali wanatarajia kupamba shoo hiyo ambayo Dj John Peter Pantelakis atalisindikiza.
    Wadhamini wa shindano hilo ni TBL Kupitia Redds wamedhamini shindano hilo sanjari na kinywaji cha Zanzi, Michuzi Media Group, Radio EFM 93.7 Cash & Carry Distributors, Kitwe General Traders, Rio Gym & Spa, CXC Africa, 88. 5 Clouds FM, City Sports Lounge, Gazeti la Jambo Leo, Kiwango Security na 100.5 Times FM.
    BMP Promotions imeshakamilisha shindano hili la 19 tangu kuanzishwa Miss Temeke chini ya undaaji wake kwa asilimia kubwa, hivyo washabiki wa Kanda ya Temeke na vitongoji vyake watarajie mabadiliko makubwa katika aina ya shindano la urembo litakavyokuwa Ijumaa.
    WALIOWAHI KUWA MISS TEMEKE TANGU 1996;
    1996- Asela Magaka
    1997- Miriam Odemba
    1998- Khamisa Ahmed (Miss Temeke anayeendea kujiita hivyo huko Marekani)
    1999- Ediltruda Kalikawe
    2000- Irene Kiwia
    2001- Happyness Sosthnes Magesse
    super model Millen( Miss Tanzania)
    2002- Regina Mosha
    2003- Hawa Ismail ( Sylvia Bahame first runner up and Miss Tanzania same year)
    2004- Cecylia Assey ( mrs Agrey Marealle), first runner up Miss Tanzania
    2005- Seba Aggrey
    2006- Jokate Mwegelo (Miss Tanzania fisrt runner up), Irene Uwoya 1st runner Temeke & 3rd runner up Miss Tanzania
    2007- Queen David ( Miss Tanzania second runner up)
    2008- Angela Lubala (top five Miss Tanzania)
    2009- Sia Ndaskoy (top five Miss Tanzania)
    2010- Genevieve Mpangala ( Miss Tanzania)
    2011- Husna Twalib
    2012- Edda Sylvester
    2013- Svetlana Nyameyo ( Latifa Mohamedsecond runner Temeke and first runner up Miss Tanzania)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NANI KUWA MISS TEMEKE LEO? SHOO LINAPIGWA TCC NA BURUDANI KIBAO ZIKIONGOZWA NA MNYAMA TID Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top