• HABARI MPYA

    Tuesday, November 11, 2014

    DAVID MOYES KOCHA MPYA REAL SOCIEDAD

    KLABU ya Real Sociedad ya Hispania imemtangaza David Moyes kuwa kocha wake mpya, licha ya Mscotland huyo kusema ni 'maajabu ya mwaka' klabu hiyo kumpa Mkataba wa miezi 18.
    Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 anafikiri majukumu aliyochukua na mazito mho katika timu hiyo ambayo haifanyi vizuri kwa sasa katika La Liga, wakati anahitaji kurejesha heshima yake baada ya kufukuzwa Manchester United Aprili mwaka huu.
    Bahati mbaya, Phil Neville alikataa kuungana naye huko kama Kocha Msaidizi na sasa anatafuta mtu mwingine wa kufanya naye kazi Hispania. Bado haijulikani sasa Moyes atamchukua nani katika benchi lake la Ufundi.  
    Kocha wa zamani wa Manchester United, David Moyes amekuwa kocha mpya wa Real Sociedad kwa mujibu wa klabu hiyo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DAVID MOYES KOCHA MPYA REAL SOCIEDAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top