• HABARI MPYA

    Saturday, March 01, 2025

    MUKWALA APIGA HAT TRICK SIMBA YAICHAPA COASTAL UNION 3-0 ARUSHA


    TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
    Imekuwa siku nzuri kwa mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Steven Dese Mukwala aliyefunga mabao yote matatu ya Wekundu wa Msimbazi leo, dakika za 30, 45’+2 na 56.
    Kwa ushindi huo, Simba inafikisha pointi 54 katika mchezo wa 22, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi nne na mabingwa watetezi, Yanga ambao pia wamecheza mechi moja zaidi.
    Kwa upande wao Coastal Union baada ya kipigo hicho wanabaki na pointi zao 24 za mechi 22 sasa nafasi ya tisa katika ligi ya timu 16.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MUKWALA APIGA HAT TRICK SIMBA YAICHAPA COASTAL UNION 3-0 ARUSHA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top