Martinez
KLABU ya Liverpool imemtaja kocha Roberto
Martinez kuziba nafasi ya Kenny Dalglish aliyefukuzwa.
Kampuni ya Fenway Sports Group (FSG) ya
Marekani, Wamiliki wa Wekundu hao wa Anfield, wamewasiliana na kocha huyo wa
Wigan, Martinez wiki iliyopita na vuanzo vinasema Msyanyola huyo ana nafasi
kubwa kukalia kiti cha Dalglish aliyefukuzwa leo.
Aprili, mwaka huu Martinez alikwishaamua
ataondoka Wigan licha ya mmiliki wa klabu hiyo, Dave Whelan kukanusha kwamba
hakuna ombi rasmi walilopokea, Liverpool sasa inatarajia kumtwaa kocha huyo
mwenye umri wa miaka 38, ambaye pia anawaniwa na Aston Villa.
0 comments:
Post a Comment