• HABARI MPYA

    Sunday, May 13, 2012

    AZAM YASAJILI KI[PA WA SIMBA, MTOTO WA PAZI ATOLEWA KWA MKOPO COASTAL


    Home
    KIPA wa Mtibwa Sugar, Deo Munishi ‘Dida’ aliyewahi kuchezea Simba SC, amesajiliwa Azam FC akiwa miongoni mwa wachezaji wawili wapya pamoja na kiungo Mkenya George Odhiambo ‘Blackberry’.
    Azam imesajili wachezaji 27- huku wanne kati yao wakiwa katika hesabu za kutolewa kwa mkopo akiwemo kiungo Zahoro Pazi anayepelekwa Coastal Union ya Tanga- maana yake itabaki na wachezaji 23.
    Jumla, Azam imesajili wachezaji wanne wa kigeni na kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu wana nafasi moja ya kusajili mchezaji wa kigeni na tayari rada za klabu hiyo zimemlenga mshambuliaji wa Simba SC, Emmanuel Okwi ambaye yuko juu hvi sasa hakuna mfano.
    Wachezaji wa kigeni wa Azam ni beki Ibrahim Shikanda kutoka Kenya, viungo Blackberry kutoka Kenya, Kipre Balou na mshambuliaji Kipre Tcheche, wote kutoka Ivory Coast.
    Aidha, Azam FC imezikata maini Simba na Yanga zilizokuwa zinamuwania beki wao, Luckson Kakolaki aliyekulia kwenye viunga vya wana Lamba Lamba, ambaye amesani wiki hii.
    Azam FC ambayo itawakilisha nchi kwenye, ambayo mwakani itacheza Kombe la Shirikisho Afrika, pia imewapandisha chipukizi wake wane kutoka timu ya vijana (U-20), ambao ni Aishi Salum, Jackson Wandwi, Dizana, Ibrahim Rajab Jeba na Joseph Kimwaga
    Kikosi kamili cha washindi hao wa Medali ya Fedha Ligi Kuu na mabingwa wa Kombe la Mapinduzi ni; Makipa Mwadini Ally, Deo Munishi, Aishi Salum na Jackson Wandwi, mabeki Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samih Haji Nuhu, Luckson Kakolaki, Said Moradi, Joseph Owino na Aggrey Morris na viungo Kipre Bolou, Abdulhalim Humud, Himid Mao, Salum Abubakar, Abdi Kassim Sadallah, Ramadhani Suleiman Chombo, Abdulghani Ghulam, Ibrahim Rajab Jeba, Jabir Aziz Stima, Ibrahim Joel Mwaipopo, Kipre Tchetche, Mrisho Ngassa, Zahoro Pazi, Khamis Mcha na George Odhiambo, wakati washambuliaji wa ni Gaudence Mwaikimba na John Raphael Bocco ‘Adebayor’.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM YASAJILI KI[PA WA SIMBA, MTOTO WA PAZI ATOLEWA KWA MKOPO COASTAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top