Owen
KIUNGO Owen Hargreaves ametemwa na klabu ya Manchester City,
baada ya msimu mmoja wa kuwa na klabu hiyo.
Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa England alitua
Etihad msimu uliopita, baada ya kumaliza mkataba Manchester United.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, amecheza mechi nne tu
kwa mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu England msimu huu, akifunga bao moja tu
katika mechi ya nyumbani na Birmingham City kwenye Kombe la Ligi, kwa shuti
kali la umbali wa mita 20.
Amekuwa akisumbuliwa na majeruhi msimu wote na klabu hiyo
imethibitisha katika tovuti yake leo kwamba kiungo huyo wa zamani wa Bayern
Munich ataruhusiwa kuondoka msimu huu.
Hargreaves amekuwa akisumbuliwa na maumivu kwa misimu michache
iliyopita, tangu akiwa Manchester United ingawa ametwaa taji la Ligi ya
Mabingwa na klabu hiyo msimu wa 2007/08.
Mzaliwa huyo wa Canada, alilazimika kumuona mtaalamu wa goti
Amerika mapema mwaka 2010 katika jitihada za kutatua tatizo lake sugu.
Kufuatia kufanyiwa upasuaji, Hargreaves alicheza mechi ya
kwanza ya Ligi Kuu baada ya takriban miaka miwili dhidi ya Sunderland, lakini
majeruhi zaidi yaliibuka.
Alicheza mechi moja zaidi akiwa na jezi ya Mashetani Wekundu
katika Kombe la Ligi dhidi ya Wolves Uwanja wa Old Trafford, Novemba mwaka huo,
lakini akalazimika kutoka nje baada ya dakika 10 za mwanzoni, kufuatia maumivu
ya nyama za paja.
Kiungo huyo, ambaye ameichezea timu ya taifa ya England
mechi 42, alihamia City msimu uliopita baada ya kutemwa na Sir Alex Ferguson,
ili akaribu bahati yake sehemu nyingine, lakini ameshindwa pia kusimama imara na
huko pia na anatemwa
0 comments:
Post a Comment