• HABARI MPYA

    Monday, June 11, 2012

    SHEVCHENKO AING'ARISHA UKRAINE

    Ukraine imeibuka na ushindi wa 2-1 katika mchezo wao wa kwanza Euro 2012, Kundi D dhidi ya Sweden, kwenye Uwanja wa NSK Olimpijs'kyj, mjini Kyiv. Sweden walitangulia kupata bao kupitia kwa Zlatan Ibrahimovic dakika ya 52, akiunganisha pasi ya K. Kallstrom, kabla ya Andrey Shevchenko kuwasawazishia Ukraine, wenyeji wa fainali hizo kwa pamoja na Poland dakika ya 55, akiunganisha pasi ya A. Yarmolenko na baadaye Shevchenko akafunga la pili dakika ya 61, pasi ya Y. Konoplyanka. Katika mechi ya awali ya Kundi D, kati ya England na Ufaransa, timu hizo zilitoka sare ya 1-1. Pichani ni Shevchenko akifunga.

    Shevchenko anafunga

    Shevchenko akishangilia moja ya mabao yake

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHEVCHENKO AING'ARISHA UKRAINE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top