• HABARI MPYA

    Sunday, February 10, 2013

    ADEBAYOR YUKO JUU YA KICHWA CHA AVB


    KOCHA wa Tottenham, Andre Villas-Boas ameshindwa kumuadhibu mshambuliaji Emmanuel Adebayor licha ya kuchelewa kurudi kwenye timu, baada ya kumaliza majukumu ya kimataifa.
    Alimtaka mshambuliaji huyo awasili saa 9:00 Alasiri Ijumaa baada ya Togo kutolewa kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika na aripoti mazoezini Tottenham.
    Togo ilitolewa Jumapili iliyopita, lakini Adebayor alichelewa kujiunga na wenzake mazoezini.
    Missing: Emmanuel Adebayor was absent from Tottenham training
    Emmanuel Adebayor hakuwepo mazoezini Tottenham jana, lakini leo kapangwa

    Licha ya kuchelewa kuripoti mazoezini, Villas-Boas alimpanga Adebayor katika kikosi cha leo kilichoibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Newcastle katika Ligi Kuu ya England.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ADEBAYOR YUKO JUU YA KICHWA CHA AVB Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top