• HABARI MPYA

    Sunday, February 10, 2013

    RONALDO ATUMA SALAMU MAN UNITED AKIPIGA HAT-TRICK REAL IKIUA 4-1 HISPANIA


    MRENO Cristiano Ronaldo ametoa onyo kali kwa klabu yake ya zamani, Manchester United kwa kufunga mabao matatu peke yake wakati Real Madrid ikipasha misuli kwa ajili ya mechi dhidi yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ilipoikung'uta mabao 4-1 Sevilla kwenye Uwanja wa Bernabeu.
    Mechi dhidi ya Sevilla have imethibitisha ubora wa Ronaldo na hakuwa na tofauti usiku wa jana akifuatiwa na Karim Benzema, akifunga bao la kwanza dakika ya 18 na mengine dakika za 26, 46 na 59, Madrid wakiibuka washindi.
    Special one: Real Madrid's Cristiano Ronaldo (C) is congratulated by team mates Fabio Coentrao and Raul Albiol after scoring a goal against Sevilla
    Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo (katikati) akipongezwa na wenzake Fabio Coentrao na Raul Albiol baada ya kufunga bao dhidi ya Sevilla jana
    Cool finish: Ronaldo scores his goal under pressure of Sevilla's Federico Fazio
    Ronaldo akifunga bao lake huku amezongwa na beki wa Sevilla, Federico Fazio

    Sasa ametimiza Hat-tricks 20 tangu ajiunge na vigogo hao wa Hispania kabla ya kupumzishwa na kocha Jose Mourinho dakika ya 63 kwa ajili ya mechi ya Jumatano dhidi ya United, ambayo itakuwa ya kwanza ya hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa.
    Granada, ambayo iliwazima vijana wa Mourinho wiki iliyopita kwa kuwalaza 1-0 kwa bao la Ronaldo kujifunga, imeendeleza ubabe, baada ya kuichapa Deportivo La Coruna mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Riazor.
    Bao la kujifunga la Carlos Marchena karibu kabisa na mapumziko liliwatia moto Granada na Ighalo akafunga la pili dakika sita baadaye kipindi cha pili.
    Kisha Depor wakapoteza nafasi kadhaa kabla ya kuwapa penalty wapinzani wap- iliyowekwa kimiani na Guilherme Siqueira - dakika ya mwisho huku Manuel Pablo akitolewa nje kwa kadi nyekundu.
    "Kwa Madrid kila mechi ni maalum, lakini kwa Jumatano tunapaswa kuwa tayari kukutana na changamoto,"alisema beki wa Madrid, Pepe, aliingia baadaye kucheza mechi yake ya kwanza tangu afanyiwe upasuaji wa kifundo chake cha mguu wa kulia mapema Januari. 
    "Cristiano amecheza vizuri. Amepambana sana, tunahitaji aendelee hivyo,".
    Three and easy: Ronaldo completes his hat-trick
    Ronaldo akikamilisha Hat-trick yake
    Off and running: Ronaldo claimed his 20th hat-trick
    Ronaldo akishangilia Hat-trick yake ya 20
    danger man: Ronaldo with a trademark free kick
    Ronaldo akifunga kwa mpira wa adhabu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: RONALDO ATUMA SALAMU MAN UNITED AKIPIGA HAT-TRICK REAL IKIUA 4-1 HISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top